Header Ads

Serikali yasema Itaendelea Kupambana na Wanaoendeleza Vitendo vya Ukeketaji



Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Sihaba Nkinga akitembelea maeneo mbalimbali katika Kituo cha Kulea Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga).

Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Sihaba Nkinga akisaini kitabu cha wageni alipofika katika Kituo cha Kulea Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) pembeni ni Mkurugenzi wa Kituo hicho Sister Stella Mgaya.

Baadhi ya watoto waliokimbia ukeketaji wakiwa katika maandano kuelekea eneo walilofanyia mahafali.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Sihaba Nkinga na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Bw. Glorious Luoga wakiwaongoza watoto waliokimbia ukeketaji kwenye maandamano wakati wa mahafali leo Tarime.


Mkurugenzi wa Kituo cha Kulea Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) Sister Stella Mgaya akiongea wakati wa mahafali mahafali ya wasichana 46 waliokimbia ukeketaji na kushukuru juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na uongozi wa wilaya ya Tarime kukabiliana na tatizo hilo na kuendelea kuomba wadau kujitokeza kuwaendeleza watoto wanaohitimu kituoni hapo.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Bi.Lydia Bupilipili akiongea wakati wa mahafali mahafali ya wasichana 46 waliokimbia ukeketaji na kuwasisitiza wazazi na walezi kubadilika na kuachana na imani potofu ya ukeketaji ili kuwawezesha kutimiza malengo yao.


Mkuu wa Wilaya ya Tarime Bw. Glorious Luoga akiongea wakati wa mahafali ya watoto waliokimbia kukeketwa na kujiunga katika kituo Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) ambapo aliwataka wazazi wanaowatenga na kuwalazimisha kuwakeketa watoto waliohitumu mafunzo kuacha tabia hiyo kwani watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Sihaba Nkinga akiongea wakati wa mahafali ya watoto waliokimbia kukeketwa na kujiunga katika kituo Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) ambapo alisisitiza kuwa serikali itaendelea kuwachukulia hatua wazazi na jamii inayoendelea na kitendo kiovu cha ukeketaji kwa watoto wa kike.

PICHA NA IDARA YA HABARI

No comments

Powered by Blogger.