Header Ads

Naibu Waziri MASAUNI akutana na Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akijibu maswali yaliyoulizwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakati wa ziara ya kikazi iliyofanyika leo jijini Mbeya.Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Kanali Mstaafu Masoud Ally.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Juliana Shonza (katikati) akizungumza wakati wa kipindi cha kuuliza maswali yaliyoelekezwa kwa Idara zilizopo ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi .Wengine ni wajumbe wa kamati hiyo.Kamati hiyo ya Bunge  iko jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.

Mkuu wa Idara ya Uhamiaji mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi , Asumsio Achachaa, akijibu maswali yaliyoelekezwa kwenye Idara yake na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama(hawapo pichani), wakati wa mkutano na kamati hiyo iliyokutana Jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.

Mkuu wa Jeshi la Magereza mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi(ACP)  Paul Kajida, akijibu maswali yaliyoelekezwa kwenye Idara yake na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama(hawapo pichani),  wakati wa mkutano na kamati hiyo iliyokutana  Jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.

(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

No comments

Powered by Blogger.