Header Ads

Naibu Waziri HAMAD MASAUNI atembelea Gereza la Ruanda Jijini Mbeya

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiongozana na Mkuu wa Jeshi la Magereza jijini Mbeya Kamishna Msaidizi Paul Kajida (kulia) wakati alipowasili kukagua shughuli za uzalishaji thamani za ndani na sabuni katika gereza la Ruanda .Naibu Waziri yupo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.

Mkuu wa Kiwanda cha Gereza la Ruanda ASP Michael Kuga, akisoma taarifa ya hali ya uzalishaji wa sabuni na thamani za ndani mbele ya Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa ziara ya kikazi ya ukaguzi wa shughuli za maendeleo zinazofanyika katika magereza yaliyopo jijini Mbeya.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wapili kushoto) akipata maelezo juu ya utengenezwaji wa kiti kinachotengenezwa na wafungwa wa gereza la Ruanda wakishirikiana na wataalamu wa Jeshi la Magereza.Naibu Waziri yupo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akiangalia moja ya sabuni zinazozalishwa na wafungwa wa Gereza la Luanda wakishirikiana na wataalamu wa Jeshi la Magereza.Kulia ni Mkuu wa Kiwanda hicho().Naibu Waziri yupo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.

(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

No comments

Powered by Blogger.