Header Ads

Ushirikiano Baina ya China na Tanzania Kuendelea Kuimarika

Waziri wa Mambo ya Mambo ya Nje wa China, Wang Yi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano wao na waandishi hao kufuatia ziara yake ya siku moja nchini. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza wakati wa kikao cha majadiliano na mgeni wake ambaye ni Waziri wa Nje wa Jamhuri ya Watu wa China alipofanya ziara ya siku moja nchini leo jijini Dar es Salaam. Waziri huyo anatarajiwa kuondoka nchini leo kuelekea DRC Congo kuendelea na ziara yake katika nchi za bara la Afrika.

Baadhi ya viongozi  kutoka China na Tanzania wakifuatilia mkutano baina ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa China na Tanzania na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam. Miongoni mwao ni Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing( wapili kulia), Katibu MKuu Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji, Dkt. Adelhelm Meru.

No comments

Powered by Blogger.