Maandalizi ya Uchaguzi Mdogo Jimbo la Dimani Mjini Zanzibar yanaendelea
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Mhe. Jaji Mstaafu Damiani Lubuva akiongoza kikao cha Wajumbe wa Tume na Sekretarieti
kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi mdogo katika jimbo la Dimani mjini Zanzibar
leo Desemba 14, 2016 ,Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Uchaguzi Bw.
Kailima Ramadhan.
Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Mhe.Jaji Mstaafu Mary Longway akizungumza jambo wakati wa kikao cha Wajumbe na
Sekretarieti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) leo Desemba 14, 2016 mjini
Zanzibar.
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Hamid M. Hamid (kushoto) akizungumza jambo
wakati wa kikao cha Wajumbe na Sekretarieti ya Tume mjini Zanzibar leo, Katikati ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Mstaafu Damian Lubuva na Mkurugenzi wa
Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhan (kulia).
Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC) Prof. Amon Chaliga akieleza jambo wakati wa kikao cha Wajumbe na
Sekretarieti ya Tume kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi mdogo wa Jimbo la
Dimani, Zanzibar, Kulia ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Mstaafu Damian Lubuva
na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Hamid M.
Hamid (katikati).
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Tume
ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe akizungumza na Wajumbe na
Sekretarieti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi mjini Zanzibar kwenye kikao cha
maandalizi ya Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani Zanzibar leo Desemba 14, 2016.
Wajumbe na Sekretarieti ya Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakiongozwa na Mwenyekiti
wa Tume Jaji Mstaafu Damiani Lubuva mjini Zanzibar leo Desemba 14, 2017. Picha/Aron Msigwa – NEC, Zanzibar.
Post a Comment