Header Ads

Everton yazidisha masaibu ya Leicester

Kevin Mirallas na Romelu Lukaku waliiweka Everton kifua mbele na kuipatia ushindi wake wa kwanza ugenini tangu mwezi Septemba huku mabingwa watetezi wa ligi wakishuka karibu na eneo la kushushwa daraja.
Winga wa Ubelgiji Mirallas alichukua fursa ya kuiweka mbele Everton baada ya safu ya ulinzi ya Leicester kufanya masikhara .
Daniel Amartey ,Leonardo Ulloa na Damarai Gray walilishambulia lango la Everton na kumpatia kazi ya ziada kipa Roble lakini Everton ikaongeza bao la pili kupitia Romelu Lukaku.
Pasi ndefu kutoka kwa Ross Barkley ilimpata Lukaku ,ambaye alionyesha umahiri wake kabla ya kupiga mkwaju uliomuacha kipa Kasper Schmeichel bila jibu.

No comments

Powered by Blogger.