Naibu Waziri, Ofisi
ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mhe.Anthony Mavunde akipokea Tuzo kutoka
kwa Mjasiriamali na Mkurugenzi wa kampuni ya Malkia Investment ltd Bi. Jenifer Shigole
aliyoshinda katika tuzo za African entrepreneurship Awards zilizofanyika nchini
Morocco na kuibuka mshindi wa kwanza katika kipengele cha masuala ya Elimu na
Mazingira na kujishindia mtaji wa dola laki moja na nusu.
...............................
Na
Daudi Manongi, MAELEZO
Naibu Waziri, Ofisi
ya Waziri Mkuu (Kazi,Vijana na Ajira), Anthony Mavunde amesema Serikali
itaendelea kuwatunza, kuwatangaza na kuwaendelea vijana wabunifu nchini ili
kuwahamasisha kufanya shughuli za ubunifu nchini.
Aliyasema hayo leo Jijini
Dar es Salaam wakati akipokea tuzo ya Mkurugenzi wa kampuni ya Malkia
Investment Ltd, Jenifer Shigole aliyoshinda katika tuzo za African Entrepreneurship
Awards nchini Morocco.
Katika shindano hilo,
Jenifer aliiibuka mshindi wa kwanza katika kipengele cha masuala ya elimu na mazingira
na kujishinda mtaji wa dola laki moja na nusu.
“Mtakumbuka Mhe. Rais
katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge alituagiza kuwatambua vijana wabunifu
na tayari tumewatambua na kuwaendeleza na natoa rai kwa vijana kujitokeza ili
waweze kushilikiana na Serikali” Alisema Mavunde.
Aidha alisema Serikali
kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana
wataikopesha kampuni ya Jenifa ya Malkia Investment Ltd kiasi cha Tsh Milioni
30 ili zisaidie kupanua mradi wake kwa lengo la kuongeza uzalishaji ili bidhaa
zake ziwafikie vijana wengi zaidi waishio vijijini.
Mavunde alisema kuwa
Serikali imeipatia kampuni hiyo ekari moja ya kiwanja kilichopo Wilayani Kibaha
Mkoani Pwani ili kujenga kiwanda cha kutengeneza pedi za kike ambazo ni
mkombozi kwa vijana wa kike hasa walio mashuleni.
Anaongeza kuwa
Serikali pia itamtambulisha kwa vijana waelimishaji wa kitaifa wa stadi za
maisha walioandaliwa na Serikali kwa
ajili ya kufundisha stadi za maisha katika mikoa ya Kagera,Mwanza, Geita,
Simiyu, Dar es salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora
na Manyara .
Kwa mujibu wa Mavunde
hatua hiyo imelenga kusaidia vijana wa kike kupata namna bora ya kutumia bidhaa
za kampuni hiyo kwa ajili ya kutunza afya zao.
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Jenister Shigole
aliishukuru Serikali kwa kutambua mchango wake na vijana wenzake kwa
kuona mchango wao katika jamii na kutoa wito kwa vijana wengi kuwa wabunifu wa
miradi mbalimbali.
Alisema kiwanda kitachotarajiwa
kuanzishwa na kampuni hiyo kitaisaidia kutengeneza ajira na kupunguza uharibifu
wa mazingira kwani pedi wanazotengeneza zimetengenezwa kwa pamba tofauti na
zingine ambazo zimetengenezwa kwa plastic.
Aidha Shigole ametoa wito
kwa vijana wengi zaidi kushiriki kupitia fursa izi za African Entrepreneurship
Awards ambayo itawasaidia kimaendeleo kwa kubuni miradi mbalimbali kupitia
uwezo na ujuzi walionao.
|
Post a Comment