Header Ads

Wasimamizi wa Uchaguzi Mdogo Wametakiwa Kuzingatia Sheria, Kanuni na Maadili

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Bw.kailima Ramadhani akifungua mafunzo ya siku 3 ya Wasimamizi wa
Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya jimbo na Kata na
Maafisa wa Uchaguzi leo mjini Dodoma.


Baadhi ya Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi
Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya jimbo na Kata na Maafisa wa Uchaguzi
wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao
wakati wa Uchaguzi mdogo utakaofanyika Januari 22, 2017 leo mjini
Dodoma.

...................................
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewataka Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi wa Uchaguzi mdogo wa Udiwani utakaofanyika katika Kata 20 za Tanzania Bara na Ubunge katika jimbo la Dimani Visiwani Zanzibar  Januari 22, 2017 kuzingatia Sheria, Kanuni na Maadili ili Uchaguzi huo uwe Huru na wa Haki.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhan wakati akifungua mafunzo ya siku 3 ya
Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya
jimbo na Kata na Maafisa wa Uchaguzi leo mjini Dodoma.

Mkurugenzi Kailima amewataka Wasimamizi hao kuzingatia matakwa ya
Katiba, Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali katika kushughulikia
mambo yatakayojitokeza wakati wa uchaguzi huo.

Katika kutimiza majukumu yao wawe tayari kutoa ufafanuzi juu masuala
mbalimbali kwa kuzingatia sheria na kutokuwa tayari kukubali
kuyumbishwa na mtu yeyote atakayekiuka  miongozo, sheria na kanuni za
Uchaguzi.

Amewataka Wasimamizi hao watende mambo yote kwa kuzingatia kanuni na Sheria na kutoa maamuzi sahihi kwa mustakabali wa Taifa na kuwasisitiza kuepuka kutoa upendeleo katika maamuzi wanayoyafanya  na wasikubali kuyumbishwa na matakwa ya baadhi ya watu.

No comments

Powered by Blogger.