Header Ads

Kijana Aliyewaua watu 5 Marekani akamatwa


Polisi katika jimbo la Florida wanamzuilia mwuaji mshukiwa baada ya watu watano kupigwa risasi na kuawa na wengine wanane kujeruhiwa katika uwanja wa ndege wa Lauderdale.
Shambulizi hilo lilitokea katika eneo la kupokea mizigo. Lengo la shambulizi hilo halijulikani.
Mshukiwa ametajwa kama Estaban Santago aliyepatikana na kitambulisho cha kijeshi na ambaye amewahi kufanya kazi Iraq.
Maafisa wa FBI katika afisi ya Alaska wamekuwa na hali ya wasiwasi kumhusu kwa sababu ya tabia zake za zisizoeleweka na mnamo Novemba walimwelekeza kwa daktari bingwa wa akili.
Polisi wanasema mshukiwa huyo hakusema lo lote kabla ya mashambulizi au baadaye. Alipoishiwa na risasi alilala chine kwa upole.


No comments

Powered by Blogger.