Header Ads

ARGENTINA na CHILE Kuvaana Tena Kwenye Fainali ya COPA AMERICA




Na Dotto Mwaibale

 Michuano ya kombe la Copa America iliyokuwa ikitimua vumbi nchini Marekani kuanzia Juni 4 na kuonekana moja kwa moja kupitia ving’amuzi vya StarTimes itamalizika siku ya Juni 27 katika fainali itakayozikutanisha tena kwa mara nyingine timu za taifa za Argentina na Chile katika uwanja wa East Rutherford, New Jersey.

Katika fainali ya mwaka jana iliyofanyika Julai 4 timu ya taifa ya Chile ambao ndio walikuwa wenyeji waliweza kutumia vizuri fursa hiyo kwa kutwaa ubingwa baada ya kuwafunga Argentina katika hatua ya mikwaju ya penati.  

Timu ya taifa ya Argentina imetinga hatua ya fainali baada ya kuibamiza Marekani magoli manne bila ya mujibu huku nahodha na mchezaji nyota Lionel Messi akivunja rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote. Messi alifikisha magoli 55 moja zaidia ya mchezaji Gabriel Batistuta aliyekuwa akiishikilia rekodi hiyo kwa muda wa miaka 15.

Chile ambao ni mabingwa watetezi nao wameingia hatua hiyo kwa kishindo na kudhihirisha kuwa hawakubahatisha hatua hiyo baada ya kuilaza timu ya Colombia magoli mawili kwa bila kupitia kwa wachezaji wake Charles Aranguiz na Jose Fuenzalida.

Wapenda soka wote ulimwenguni wanatarajia kuona fainali kali na ya aina yake baina ya timu hizo hususani ushindani mkali kutoka kwa kikosi cha Argentina kilichopo kwenye ubora wa hali ya juu kikiongozwa na nyota wake Lionel Messi huku kikiwa na kiu kubwa ya ubingwa kwa takribani muda wa miaka 23.

Pia mashabiki wanasubiria kwa hamu kuona Lionel Messi kama ataweza kuiongoza timu yake kutwaa kombe hilo na pia kuchukua ufungaji bora kwa kumzidi mchezaji wa Chile Eduardo Vargas mwenye magoli sita huku yeye akiwa na matano.


No comments

Powered by Blogger.