Header Ads

Rais Dkt JOHN MAGUFULI akabidhi Shilingi Milioni 10 Kusaidia Upanuzi wa Kanisa Wilayani CHATO

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Sakramenti takatifu kutoka kwa Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Chato Padre Henry Mulinganisa.

Na Mwandishi Maalumu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa Mchango wa Shilingi Milioni 10 kwa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita kwa ajili kuchagia upanuzi wa kanisa hilo.

Fedha hizo zimekabidhiwa na Kaimu Mnikulu Bw. Ngusa Samike katika misa ya pili ya ibada ya Jumapili ya pili ya Pasaka, iliyofanyika kanisani hapo leo tarehe 03 April, 2016.

Kabla ya misa hiyo ya pili Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwa pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya Mheshimiwa Raila Amoro Odinga na Mkewe Mama Ida Odinga, walisali misa ya kwanza ambapo Rais Magufuli aliahidi kuchangia shilingi milioni 10 kwa ajili ya upanuzi wa kanisa hilo ambao unaendelea.

Katika Misa hiyo Paroko wa Parokia ya Chato, Padre Henry Mulinganisa alieleza kuwa kanisa hilo linatarajia kuadhimisha miaka 50 ya tangu kuanzishwa kwake baadaye mwaka huu, na kwamba maadhimisho hayo yanakwenda sambamba na upanuzi wa kanisa ambao unachangiwa na waumini wenyewe.


Padre Mulinganisa amemshukuru Rais Magufuli kwa mchango huo, na amemuahidi kuwa utatumika vizuri ili uendeleze upanuzi wa kanisa hilo pamoja na michango ya waumini wengine.

No comments

Powered by Blogger.