Header Ads

Makamu wa Rais SAMIA SULUHU amfuta Machozi MILLEN MAGESE mapambano Dhidi ya ENDOMETRIOSIS

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Mama Samia Suluhu amemfuta machozi Mwanadada, Happiness Millen Magese ambaye ni shujaa wa kipekee kutoka Afrika dhidi ya mapambano ya ugonjwa wa Endometriosis.

Mama Samia amechukua hatua hiyo jioni ya 15 Aprili 2016 wakati wa hafla maalum ya kumkabidhi tuzo.

Katika kilio chake hicho, Millen kimemfanya Mama Samia kumfuta machozi na kumpa kitambaa, mwanamitindo huyo huku akimweleza kuwa, Serikali itaendelea kushirikiana naye kwani tatizo hilo si la Millen pekee bali ni kwa wanawake wengi hapa Tanzania.

Mama Samia alimwambia kuwa, tatizo alilonalo la kuziba kwa mirija ya uzazi lipata ufumbuzi na kutaka asilie kwani Serikali inania njema kwa watu wake hivyo wataendeleza juhudi Zaidi huku akifungua milango na mwanadada huyo.

Suluhu alisema kuwa hata yeye tatizo kama hilo lipo katika familia yake, lakini ana amini kwa ushirikiano wa mwanamitindo huyo tatizo hilo linapewa uzito. Alisema kuwa ni kitu kilichokuwa kikimuumiza sana kichwa, ana amini kupitia Millen hata binti yake atapata nafuu.

"Nimefurahi kukutana nawe na Serikali haitakuangusha tutakuunga mkono katika kuhakikisha gonjwa hili linapata ufumbuzi na kutoa elimu kwa kila mtanzania kulitambua"alisema.

Akizungumza kwa upande wake Magese alisema amekuwa akifanya semina mbalimbali kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa Hospitali ya Taifa, Muhimbili, kuwaelimisha wanawake kuhusu endometriosis.

Alisema Machi 30, mwaka huu Taasisi ya Millen Magese ilikusanya vijana (hususani wa kike) wapatao mia tano kutoka shule za Mugabe, Manzese, Salma Kikwete na Turiani, kuwafundisha, kuwatahadharisha na kuwatanabahi kuhusu Afya, Uenendo, Maisha yao ya kila siku na Changamoto zilizo mbele yao na hususani ikilenga zaidi watoto wa kike ambao wao ndio wahanga wa ugonjwa wa Endometriosis.

Magese alisema watoto hao wakiwafikia hata wenzao 20 tu kila mmoja basi takribani watu elfu kumi watakuwa wamefikiwa.

Tazama tukio hilo: 
DSC_1435Mwanadada Sofia Banakwa (kushoto) wakijadiliana jambo na Mwanadada Leila pamoja na Millen. wakati wa tukio hilo.

DSC_1374Mshehereshaji Matukio Chuma (kushoto) akiongoza shughulo hiyo..

DSC_1243Mwanadada Sofia Banakwa ambaye ni rafiki mkubwa wa Millen akitoa ushuhuda wa namna alivyomfahamu Millen tokea wakisoma shule moja miaka nyuma.

DSC_1252Mbunifu wa mavazi Mustafa Hassanali akitoa ushuhuda kwa Makamu wa Rais, Mh. Mama Samia Suluhu wakati wa tukio hilo lililofanyika katika ofisi na makazi ya Rais jijini Dar es Salaam. Mustafa ni miongoni mwa wabunifu wa mavazi wakongwe ambao wameweza kufanya kazi na kuwa karibu na mwanadada Millen Magese katika kampeni za mapambano wa ugonjwa wa Endometriosis.

DSC_1259. Mwanamitindo Mtanzania anayefanya shughuli zake nchini Marekani, Daxx_cruz akitoa shukrani zake kwa Mama Samia (Hayupo pichani) wakati wa tukio hilo.

DSC_1262Ruge Mutahaba akitoa shukrani zake kwa Mama Samia (Hayupo pichani) wakati wa tukio hilo, Kwa mujibu wa Millen alimwelezea Ruge "Kaka Mkubwa" kuwa ni miongoni mwa watu wanaosaidiana naye katika mapambano ya Endometriosis.

DSC_1265
Mwanadada Jokate Mwegelo akitoa shukrani zake wakati wa tukio hilo. Jakate ni rafiki mkubwa Millen ambapo alimwelezea kuwa, ataendelea kusaidiana na Millen muda wote kwani anatambua harakati za ugonjwa huo ni mkubwa.

DSC_1292
Mmoja wa wazazi wa Millen Magese akitoa ushuhuda wa namna wanavyoweza kumsaidia mtoto wao katika mapambano ya ugonjwa huo..

DSC_1280Dk.Kairuki akitoa maelezo ya namna anavyoufahamu ugonjwa huo wa Endometriosis.

DSC_1275 DSC_1274Mwandada Millen akiwa pamoja na Mama Samia wakati wa tuki hulo. Kushoto ni Katibu wa Makamu wa Rais.

DSC_1282Millen akimuonyesha Mama Samia eneo linalomsumbua katika tatizo lake hilo.

DSC_1323Mama Samia akieleza namna walivyopokea tatizo hilo la Millen ambapo amemweleza kuwa Serikali itaendelea kupambana nalo tatizo hilo hivyo kumuakikishia Millen na taasisi yake kumuunga mkono.

DSC_1326Mama Samia akimfuta machozi Millen ambapo alimwelezea kuwa kwa sasa asiie tena kwani Serikali itahakikisha inapambana na ugonjwa huo ilikusaidia wanawake wengi hapa nchini..

nightofhope17Mama Samia akiangalia moja ya tuzo hiyo..

DSC_1337Millen Magese akimkabidhi tuzo yake hiyo Mama Samia wakati wa tukio hilo.

DSC_1361Mama Samia akiwa katika picha pamoja na rafiki wa Magese na wageni wengine waliojumuika katika tukio hilo..

DSC_1352Mama Samia akipata picha ya pamoja na familia ya Millen Magese.

DSC_1347Mama Samia Suluhu akiwa na Millen Magese na rafiki zake wakati wa tukio hilo..

DSC_1364Mustafa akiwa pamoja na Mama Samia na Millen.

DSC_1371
Baadhi ya Madaktari ambao ni wataalam wa kushughulikia tatizo la Endometriosis akiwemo Dkr. Kiiruki wakiwa katika picha ya pamoja na Mama Samia na Millen Magese.

DSC_1400DSC_1367
Kaka wa Millen Magese akiwa akipata picha pamoja na Mama Samia na marafiki wengine wakiwemo.

DSC_1376Baadhi ya waandishi wa Habari wanawake wakiwa katika picha ya pamoja na Mama Samia pamoja na Millen wakati wa tukio hilo.

DSC_1387Baadhi ya wanahabari wa kiume wakiwa katika picha ya pamoja na Mama Samia pamoja na Millen wakati wa tukio hilo lililofanyika jijini Dar es Salaam katika makazi Makamu wa Rais. (Picha zote na Andrew Chale,).

No comments

Powered by Blogger.