Header Ads

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya KILIMO, MIFUGO na MAJI yaridhishwa na Matumzi ya Fedha Mtambo wa Ruvu Chini

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji imeridhishwa na
matumizi ya fedha kiasi cha shilingi Bilioni 141 zilizotolewa na
Serikali kugharamia mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba la maji kutoka
Mtambo wa Ruvu Chini,wilayani Bagamoyo kwenda jijini Dar es salaam
kufuatia ujenzi wake kukamilika.

Akizungumza mara baada ya Kamati hiyo kutembelea maeneo mbalimbali ya
mradi huo ikiwemo mtambo wa Maji wa Ruvu Chini ulioko Bagamoyo mkoani
Pwani, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la
Hanan'g Mhe. Mary Nagu amesema kuwa kamati kamati yake  imeridhishwa
na ubora wa  kazi iliyofanyika chini ya Usimamizi wa Mamlaka ya Maji
Safi na Maji Taka Dar es salam ( DAWASA).

Amesema mradi huo wenye urefu wa kilometa 56  umekamilika na kueleza
kuwa itakua historia kwa wananchi   wa Dar es salaam waliounganishwa
na mtandao wa mabomba ya DAWASCO kukosa maji.


 Meneja wa Mtambo wa Maji wa Ruvu Chini Mhandisi Emmanuel
Makusa (katikati) akiwaongoza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Kilimo, Mifugo na Maji kutembelea Mtambo wa Maji wa Ruvu
Chini,wilayani Bagamoyo  kujionea maendeleo yaliyofikiwa kufuatia
kukamilika kwa ujenzi wa bomba lenye urefu wa Kilometa 56 linalotoka
katika mtambo huo kwenda jijini Dar es salaam.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na
Maji wakiangalia mitambo ya kuchujia maji kutoka mto Ruvu kwenye
Mtambo wa maji wa Ruvu Chini.
Sehemu ya kuchujia maji katika mtambo wa Ruvu Chini.

No comments

Powered by Blogger.