Header Ads

Polisi Afrika Kusini wampata Mtoto wa mwezi Mmoja aliyetoweka

Polisi nchini Afrika Kusini wanasema kuwa mtoto mchanga aliyekuwa ametekwa nyara ndani ya gari la mamake siku ya Ijumaa mjini Durban, amepatikana akiwa salama
Watu watatu wamekamatwa kuhusiana na uhalifu huo.
Msemaji wa polisi katika eneo la KwaZulu-Natal Luteni-Kanali Thulani Zwane, amethibitisha kuwa mtoto huyo alipatikana usiku wa manane kuamkia Jumapili.
Polisi walikuwa wakifuatilia vidokezo, ambapo baadaye viliwafanya kumpata ndani ya gari lililokuwa limeegezwa nje ya jumba la Mariannhill Toll Plaza.
Mtoto huyo wa mwezi mmoja anafahamika kama Siwaphiwe Mbambo.
Tangu siku ya Ijumaa polisi wamekuwa wakimtafuta mtoto mmoja aliyetoweka, baada ya gari la familia yao kutekwa nyara katika eneo la Durban.
Kisa hicho cha utekaji kiliwashtua watu wengi nchini humo na kuwafanya maelfu ya watu kutuma ujumbe kwenye mitandao ya kijamii ya Twitter kutoa habari aliko mtoto huyo.
Mtoto huyo mwenye umri wa mwezi mmoja, Siwaphiwe Mbambo, alikuwa katika kiti cha nyuma cha gari la mamake, pale gari hilo lilipotekwa na wanaume wawili waliokuwa na silaha nje ya duka moja kubwa la kununua bidhaa.

No comments

Powered by Blogger.