Header Ads

Issa Hayatou apigwa Chini Urais wa CAF na Ahmad ahmad wa Madagascar

Rais wa chama cha soka cha Madagascar Ahmad Ahmad ameushtua ulimwengu wa soka baada ya kumbwaga Issa Hayatou ambaye alikuwa rais wa muda mrefu wa shirikisho la soka Afrika na kushinda urais wa Caf leo March 16, 2017.
Uchaguzi uliomalizika Addis Ababa umempa ushindi Ahmad Ahmad baada ya kupata kura 30 dhidi ya 20 za Issa Hayatou.
Matokeo hayo yanahitimisha miaka 29 ya utawala wa Hayatou kama kiongozi wa juu wa soka la Afrika.
Mipango na mbinu kabla ya uchaguzi zimepelea kuwashangaza wengi baada ya kushuhudia kambi ya Hayatou ikidondoshwa.
Hayatou mwenye miaka 70 sasa, alikuwa rais wa CAF tangu mwaka 1988 wakati huo Lionel Messi akiwa na miezi tisa tu tangu azaliwe wakati mtawala huyo mzaliwa wa Cameroon alipotangazwa kusimamia soka la bara la Afrika.
Alianza kutawala tangu March 10, 1988 alikuwa anaifukuzia rekodi ya kuendelea kusalia madarakani kwa awamu ya nane mfululizo.
Uchaguzi ulifanyika leo baada ya mkutano mkuu wa 39 huko mjini Addis Ababa.
Ahmad, who appeared very emotional, becomes only the seventh Caf president in the body’s 60-year history.
Ahmad anakuwa rais wa saba wa CAF kwenye historia ya shirikisho hilo lenye miaka 60 hadi sasa tangu kuanzishwa kwakwe.

No comments

Powered by Blogger.