Header Ads

Raia wa Kigeni 4792 Wakamatwa kwa Kukiuka Sheria za Uhamiaji

Frank Mvungi-Maelezo

Takribani raia 4792 wakigeni wamekamatwa  kwa kukiuka sheria, Kanuni na Taratibu za Uhamiaji katika kipindi cha Januari hadi Aprili mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar essalam na Kaimu Kamishna wa Idara ya Uhamiaji Bw. Abass Irovya wakati wa mkutano na Vyombo vya habari uliolenga kutoa taarifa ya Operesheni mbalimbali zinazotekelezwa na Idara hiyo.

Irovya  amesema kuwa Idara hiyo imekuwa ikiendesha Operesheni ondoa uhamiaji haramu tangu mwezi Desemba mwaka jana na imeonyesha mafanikio ambapo raia1796  wamefukuzwa nchini kwa kukiuka sheria za uhamiaji.

“Wananchi walio wengi wamekuwa wakitoa ushirikiano kwa Idara yetu kutokana na uelewa wao kuongezeka kwa sababu tunayo program  ya kutoa elimu kwa umma na imeonyesha mafanikio makubwa”alisisitiza Irovya.

Bw. Irovya aliongeza kuwa waliohukumiwa kifungo ni raia 132 na 383 kesi za o zinaendelea kwenye mahakama  katika  Mikoa mbalimbali hapa nchini.

Raia 388 walilipa faini hali iliyochangia kuongeza mapato ya Serikali kutokana na kukiuka sheria na Kanuni za Uhamiaji hapa nchini.

Kwa upande mwingine kesi 509 zinaendelea katika mahakama mbalimbali hapa nchini na raia294 waliachiwa huru kutokana na mahakama kutowatia hatiani.

Idara ya Uhamiaji ina Vituo takribani 60 katika Mikoa Mbalimbali hapa nchini baadhi vikiwa  katika  Mikoa ya Tanga, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Katavi, Kigoma, Simiyu ambapo Idara hiyo imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu athari za raia wa kigeni wanaoingia nchini bila kufuata sheria na taratibu za Uhamiaji.



No comments

Powered by Blogger.