Header Ads

Usaili wa Maisha Plus wafanyika Mkoani MTWARA

Ni asubuhi tulivu katika fukwe za bahari ya hindi kusini mwa Tanzania ambapo vijana wengi wamejitokeza kufanya usaili wa mashindano ya Maisha Plus East Africa 2016. Wapo wanaoonekana kujiamini na wengine wamejawa uoga. "Ni siku niliyoisubiri kwa hamu sana" anasema Faustine Komba miongoni mwa washiriki kutoka Mtwara.

678A0009
Safari ya msimu wa tano wa mashindano ya Maisha Plus imeanza rasmi kwa kuanza na usaili uliofanyika katika hotel ya NAF Beach iliyoko Mtwara. Washiriki kutoka mikoa ya jirani nao pia walijitokeza. "Maisha Plus kwangu ni ndoto ya muda mrefu sana, niliposikia mnakuja Mtwara nikasema piga ua lazima nishiriki" Anasema Ismail Likando aliyesafiri kutoka Lindi.

678A0022
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.

678A9916
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.

678A9980
Mshiriki Grace Pemba akijifuta machozi.
Wakati usaili ukiendelea hali ya kujaa kwa maji baharini ilitokea na kulazimisha timu ya Maisha Plus kubadili utaratibu wa awali wa upigaji picha.

678A0075
Waandaaji wa mashindano ya Maisha Plus wakibadili utaratibu wa awali wa kupiga picha baada ya maji kujaa.

678A0046
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.

678A0056
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.

678A0281
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.

678A0279
Muhitimu wa shahada ya kilimo William Mbaga alibanwa kutoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ikiwemo faida za kilimo cha 'greenhouse' pamoja na namna ambavyo maziwa ya mtindi yanapatikana,William alijieleza kwa ujasiri.

678A0157
William Mbaga akiondoka baada ya kufanya usaili.
Washiriki wenye fani na ujuzi mbalimbali walijitokeza wakiwemo madereva bodaboda, mafundi, waigizaji, waimbaji, wasusi n.k

No comments

Powered by Blogger.