Header Ads

Sikubaliani na Hoja ya LOWASSA Kujiengua CCM na Kujiunga CHADEMA/UKAWA

Dr.Slaa pengine ndiye mwanasiasa wa upinzani anaeheshimika na kusikilizwa zaidi Tanzania.

Yote hii ni sababu ya misimamo yake kupinga ufisadi, kusimamia na kutetea maslai ya Taifa bila kuogopa.

Amewahi kutaja hadharani listi ya mafisadi 11 Lowasa akiwa namba tisa na Kikwete akiwa namba kumi na moja.

Alienda kule Arumeru alimtuhumu Lowasa waziwazi kwa ufisadi na kukwepesha miradi ya Arumeru na kuipeleka Monduli.

Lakini leo tunaambiwa kuwa Lowasa anakaribishwa ndani ya Chadema na kuungama dhambi na atasamehewa.

Sina tatizo na ujio wa Lowassa ndani ya chama tatizo langu ni heshima na taswira ya Dr. Slaa aliyojijengea kwa muda mrefu kwa kuukemea ufisadi.

Je leo yupo tayari kutangaza hadharani kuwa Lowasa amekuwa msafi sio fisadi tena, yupo tayari kupunguza ile list of shame ya Mwembeyanga kutoka kumi na moja na kubaki kumi.?

Japo siasa hazina adui wa kudumu wala urafiki wa kudumu, kwa hili naona heshima ya Dr.Slaa na Chadema kwa ujumla ikiporomoka.

Maana heshima ya Dr Slaa na Chadema imejengwa kwa kuukemea ufisadi, lakini tunakoelea Hali itabadilika na kuwa Chadema ni chama cha kuwasafisha Mafisadi.

Nb.Ni mtazamo tu wadau msijenge chuki.

No comments

Powered by Blogger.