Header Ads

MEYA KAPUNGA KUTETEA KITI CHAKE CHA UMEYA JIJI LA MBEYA


Na Mwandishi wetu,Mbeya
 
ALIYEKUWA Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga  ametangaza kutetea nafasi yake ya kiti cha udiwani kupitia Kata ya Itiji ndani ya Jiji la Mbeya.
Ujio wa Kapunga tena, umeonyesha kuwashtua wananchi wa eneo hilo pamoja na baadhi ya wakazi wa Jiji la Mbeya, ambao kupitia maoni yao walidai kwamba mgombea huyo alipaswa kupumzika na nafasi hiyo kuwaachia vijana.
Akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kata ya Itiji waliokusanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM wa Kata hiyo, Kapunga alisema ameamua kuitetea nafasi hiyo lengo likiwa ni kutimiza malengo yake aliyojiwekea ya kuwafikishia maendeleo wakazi wa eneo hilo.
Amesema, katika kipindi chote alichokuwepo madarakani, ameweza kutimiza na kutatua changamoto mbalimbali za maendelei na kubakia asilimia chache ambazo endapo wananchi hao watampa ridhaa ya kuwaongoza kwa mara nyingine tena basi atamalizia kipande kidogo kilichobakia.
Amesema, katika kipindi chote alichobahatika kuwakilisha wanaitiji alifanikiwa kutatua changamoto mbalimbali kama vile maji, elimu kuboresha miundombinu ya barabara katika kiwango cha vumbi.
Amesema, kutokamilika kwa ujenzi wa kituo cha afya kulitokana na eneo lililopangwa kujengwa kituo hicho kuwa na mgogoro kati ya watendaji wa halmashauri ya Jiji na wafanyabiashara wadogo ambao walikuwa wakilitumia eneo hilo kama soko la wakulima.
Amesema, wafanyabiashara hao wamekuwa wakiamini kuwa eneo hilo ni halali kwao kwa kuendeshea biashara zao jambo ambalo ni kinyume na utaratibu kwani eneo hilo lilikuwa ni machinjio ya zamani ya ng’ombe kabla serikali ya kuihamishia eneo la Veta. 
Amesema, mazungumzo yalikuwa yakiendelea kufanyika jinsi ya kulirudisha eneo hilo na kubadilisha matumizi kwa kujenga kituo cha afya hivyo anaamini endapo atapatiwa nafasi nyingine atatekeleza ahadi hiyo ya kuwafikishia karibu huduma ya afya wakazi wa Itiji.
Aidha, akizungumzia ujenzi wa barabara katika kiwango cha lami, Kapunga alisema kuwa barabara za eneo hilo hazikuingizwa kwenye mradi wa barabara uliokuwa ukifadhiliwa na Benki ya Dunia lakini tayari serikali ilikuwa ikitafuta fedha za kuona ni jinsi gani barabra za eneo hilo zitaboreshwa kutoka kiwango cha vumbi na kufikia lami.
Hata hivyo, Kapunga hakusita kuwatupia lawama baadhi ya viongozi wenzake wa chama cha mapinduzi kwa kushindwa kutoa ushirikiano kwake jambo ambalo limesababisha yeye kutupiwa lawama na wananchi wa eneo hilo na wakazi wa Jiji la Mbeya.

JAMII MOJA BLOG

No comments

Powered by Blogger.