Header Ads

SERIKALI YASAINI MKATABA WA KUKUSANYA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 12

mail.google.com 
Baadhi ya viongozi na watendaji wa Wizara ya Fedha na TRA wakati wa hafla ya kusaini Mkataba wa Makubaliano ya kukusanya mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ambayo yanakusanywa kwa mara ya kwanza nchini.

(Habari Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
……………………………………..
Serikaki imesainiana Mkataba wa Makubaliano ya kukusanya Sh. Milioni 12,362,969 za mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2015/2016 ambayo yanakusanywa kwa mara ya kwanza nchini. 
  Mkataba huo wa makubaliano umesainiwa leo jijini Dar es Salaam kati ya Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bernard Mchomvu kwenye hafla iliyohudhuriwa na baadhi ya viongozi na watendaji wa Wizara ya Fedha na TRA.
  “Hakikisheni mnakusanya mapato kama ilivyopangwa na kufikia malengo tuliyojiwekea katika kukusanya mapato ya ndani katika mwaka huu wa fedha” alisema Waziri wa Saada.
  Waziri huyo aliwaasa watendaji wa TRA kuwawekea wafanya kazi mazingira mazuri ya kutekeleza wajibu wao inavyopaswa na wanapokwenda kinyume na makubaliano ya kazi watawajibishwa kwa mujibu wa sheri, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.
  Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRA Bernard Mchomvu alimhakikishia Waziri wa Fedha kuwa watafikia lengo walilokubaliana kukusanya na hata kuzidi kiwango hicho ambacho kimeainishwa katika bajeti ya Serikali.

No comments

Powered by Blogger.