Header Ads

Chelsea, Man U kukutana Robo Fainali FA

Ratiba ya michezo ya robo fainali ya Kombe la FA imetolewa ambapo Chelsea itacheza na Manchester united, Middlesbrough itakutana na kati ya Huddersfield na Manchester City, tottenham itakutana na Millwall na Suton uso kwa uso na Arsenal au Lincoln.
Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho amesema Chelsea inapeleka nguvu zake kwenye Kombe la FA kwa kuwa ''tayari ni mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza''.
Mourinho amesema '' itanibidi kucheza na Saint Etienne na kucheza fainali Kombe la EFL na nina matumaini ya kucheza na mpinzani mwingine kwenye ligi ya Europa.ninahitaji kupambana kupata nafasi kati ya nne za kwanza kwenye ligi kuu.
Michezo hii itachezwa kati ya tarehe 11 na 12 ya Mwezi March.

No comments

Powered by Blogger.