Shule hiyo ambayo ina wanafunzi mpaka wa darasa la tano, ilikuwa na madarasa mawili tu jambo lililosababisha shughuli za utoaji elimu kwa wanafunzi kuwa ngumu.
Katika kuhakikisha changamoto hiyo inatatuliwa, Mkuu wa Wilaya akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Longido Bw. Jumaa Mhina wamefanya kazi ya ujenzi kwa kushirikiana na wananchi siku nzima ya leo.
Katika hatua nyingine mkuu huyo wa Wilaya ya Longido aliendesha harambee iliyofanikisha kupatikana kwa jumla ya shilingi milioni 10.
Post a Comment