Header Ads

Shilingi Milioni Moja Inahitajika Kuokoa Maisha ya Mtoto EBENEZA PEMBE anayesumbuliwa na Kansa ya Ngozi

Mama ROIDA MUHAMA mkazi wa Mkimbizi mjini Iringa, anamuuguza mwanaye aitwaye EBENEZA PEMBE anayesumbuliwa na saratani ya ngozi kwa miaka sita sasa.

Anaomba msaada wa hali na mali ili aendelee kumtibia mwanaye, Anahitaji kiasi cha fedha shilingi milioni moja kwa ajili ya kuendelea na matibabu katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.

Kwayeyote atakayeguswa tuma mchango wako kwa njia ya M-pesa 0767834377 au Tigo pesa 0717353529 kwa SILVANUS KIGOMBA au 0762 174 573 ROIDA MUHAMA (Mama wa Ebeneza)

Mtoto EBENEZA PEMBE anayesumbuliwa na Kansa ya Ngozi kwa zaidi ya Miaka 6 anahitaji Msaada wa fedha zitakazo muwezesha kwenda kupatiwa Matibabu katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Mtoto EBENEZA PEMBE aliyevaa shati la Bluu akiwa amebebwa na Mama yake Mzazi Bi ROIDA MUHAMA mkazi wa eneo la  MKIMBIZI manispaa ya Iringa, kushoto ni mtoto mwingine wa Bi ROIDA wakiwa katika Picha ya Pamoja.
...................

Nimeguswa na maumivu na mateso anayoyapata mtoto Ebeneza kwa zaidi ya miaka 6 nimejitolea kusaidia kusambaza taarifa za Ugonjwa wake ili kukusanya michango kwaajili ya matibabu yake.
Naomba ushirikiano wenu rafiki zangu na Mungu awabariki sana.

No comments

Powered by Blogger.