Header Ads

Ofisi ya Waziri Mkuu yawasilisha Utekelezaji wa Miradi Inayoiratibu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akitoa ufafanuzi wa utekelezaji wa shughuli za Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa Mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria katika Ukumbi wa mikutano wa  Ofisi ya Waziri Mkuu Machi 31, 2016.
Makatibu Wakuu Ofisi ya Waziri Mkuu (wa kwanza kulia) Erick Shitindi (Kazi na Ajira), Dkt. Hamis Mwinyimvua (Sera) na kushoto ni Mussa Uledi (Bunge) wakifuatilia hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria (hawapo pichani) walipokutana na ofisi hiyo tarehe 31 Machi, 2016.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe.Najma Giga (kushoto) wakati kamati hiyo ilipokutana na Ofisi ya Waziri Mkuu katika Ukumbi wa Ofisi hiyo tarehe 31 Machi, 2016.
Mratibu wa Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini Bw. Walter Swai akiwasilisha utekelezaji wa programu hiyo inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu katika mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria   katika Ukumbi wa mikutano wa  Ofisi ya Waziri Mkuu Machi 31, 2016.
Mkurugenzi wa Idara ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig.jen. Mbazi Msuya akiwasilisha masuala ya menejimenti ya maafa  katika mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria katika Ukumbi wa mikutano wa  Ofisi ya Waziri Mkuu Machi 31, 2016.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Rashidi Shangazi (mb) akichangia hoja wakati Kamati hiyo ilipokutana na Ofisi ya Waziri Mkuu katika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo Machi 31, 2016.

No comments

Powered by Blogger.