Header Ads

Kwanini Agizo la IGP Ernest Mangu Linapuuzwa..?

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu.

Na:George Binagi

Kwa muda mrefu kumekuwepo na malalamiko kwamba waendesha bodaboda nchini wamekuwa hawatii sheria za usalama barabarani, hali ambayo imekuwa ikisababisha ongezeko la ajali zinazoweza kuzuilika.

Hali hiyo ilimsukuma Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu mwishoni mwa mwezi uliopita, kutangaza Oparesheni kamata bodaboda wasiotii sheria za usalama barabara nchini nzima katika kikao kazi kilichowahusisha Maofisa Wakuu wa Polisi nchini wakiwemo Makanda wa Polisi Mikoa, Vikosi na Makao Makuu, kilichofanyika Jijini Dar es salaam.

“Pamoja na kuendelea kudhibiti uhalifu wa aina zote, natoa maelekezo kwa kila Mkoa kuhakikisha unaendesha oparesheni kali dhidi ya bodaboda ili kupunguza ajali zinazosababishwa na bodaboda ambao hawataki kufuata sheria na kanuni za usalama barabarabi”. 

Alisema IGP Mangu na kuainisha makosa yatakayosababisha bodaboda kukamatwa kuwa ni pamoja na Kubeba Mishikaki (abiria zaidi ya mmoja), Kutovaa kofia ngumu (helment) pamoja na kupita katika taa za barabarani huku taa nyekundu zikiwa zinawaka.

Soma Zaidi HAPA.

No comments

Powered by Blogger.