Header Ads

Naibu Waziri wa Habari Bi ANASTAZIA WAMBURA akutana na Asasi za Kiraia

Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura akimsikiliza kiongozi wa msafara  wa Asasi za Kiraia toka mkoani Mtwara Dkt. Lillac Malumbo aliyesimama wakati asasi hizo zilipomtembelea ofisini kwake kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya mila na desturi zilizopitwa na wakati za mkoa huo.
Katibu wa msafara Bi. Rhobi Elias kushoto akimkabidhi risala Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura inayoelezea mila na desturi hatarishi na zilizopitwa na wakati zinazoendelea kutumika katika Mkoa wa Mtwara, mila hizo ni pamoja na kuwapeleka watoto wa kike kwenye unyago wakiwa na umri mdogo, na ndoa za umri mdogo.(Picha na Benjamin Sawe-WHUSM)
Katibu wa msafara Bi. Rhobi Elias akisoma risala kwa mgeni rasmi hayupo pichani kuhusiana na mila na desturi hatarishi na zilizopitwa na wakati zinazoendelea kutumika katika Mkoa wa Mtwara, mila hizo ni pamoja na kuwapeleka watoto wa kike kwenye unyago wakiwa na umri mdogo, na ndoa za umri mdogo.

No comments

Powered by Blogger.