Header Ads

Kituo cha Mabasi MASASI sasa Safi, Wahusika Waamka baada ya Kumulikwa

Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani Wilayani Masasi yaendelea Kuboreshwa kwa kufanyiwa Usafi wa Hali yajuu.


Leo hii Baada ya Kamera yetu kupita majira ya asubuhi ilikuta eneo hilo ambalo hapo jana lilikuwa limetapakaa Uchafu wa Kila aina likiwa Safi Kabisa.


Hii inaonesha kabisa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Masasi amedhamiria kuepuka aibu ambayo ilikuwa inakuja siku za usoni kwani eneo hilo lipo katikati ya Mji huo hivyo kuonekana kirahisi na Kuleta Picha mbaya.



Tunaipongeza Halmashauri ya Mji ambayo imelichukua jambo hili kwa Umakini mkubwa hadi kufikia Kuweka Greda ambalo lilikutwa likifanya kazi ya kuendelea kuweka Mazingira sawia katika Stend kuu hiyo.

UNAWEZA BOFYA PLAY KUTAZAMA VIDEO HAPO CHINI

HONGERENI SANA...!!!

No comments

Powered by Blogger.