Header Ads

Waziri wa Habari NAPE NNAUYE ashiriki Mbio za KILIMANJARO MARATHONI 2016


 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akisalimiana na wakazi wa mji wa Moshi waliojitokeza kwa wingi kushiriki mbio za Kilimanjaro Marathon 2016 ambapo mwaka huu zaidi ya watu elfu 8 walishiriki kutoka nchi mbali mbali ambapo kati ya hao 200 walitoka nchini Kenya. 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akikimbia kwenye riadha ya Kilimanjaro Marathon 2016 ambapo alikimbia kilomita 5 pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Hai Mhe. Anthony Mtaka, mashindano hayo ya riadha yameshirikisha zaidi ya nchi 40.

 Mshindi wa kwanza wa kilometa 42.2 Kiprotich Kirui akiinua mikono juu kama ishara ya kushangilia ushindi wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2016.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akisoma risala mara baada ya kuhitimisha mbio za Kilimanjaro Marathon ambapo aliwapongeza wahiriki wote, wadhamini na kuwataka Watanzania kutumia mbio hizo kama fursa ya kuutangaza utalii uliopo nchini.

No comments

Powered by Blogger.