Header Ads

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi NAPE NNAUYE afungua Mafunzo kwa Watumishi wa CCM Makao Makuu

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akizungumza na watumishi wa Chama Cha Mapinduzi Ofisi Ndogo Lumumba wakati wa ufunguzi wa  Mafunzo maalum kwa watumishi hao wa CCM Makao Makuu Ofisi Ndogo Lumumba.

 Sehemu ya Watumishi kutoka ofisi ndogo makao makuu ya CCM Lumumba wakimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye.

 Mtumishi wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Rose Mbwali akitoa neno la shukrani baada ya Mhe. Nape Nnauye kutoa hotuba ya ufunguzi wa mafunzo ya watumishi wa CCM Makao Makuu, Ofisi Ndogo Lumumba.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye (katikati) akiwa pamoja na Mkufunzi wa Mafunzo kwa Watumishi Ndugu Saidi Sizya (kulia) na Mkuu wa Utawala na mratibu wa mafunzo hayo Bi. Mwajuma A. Nyamka wakisikiliza baadhi ya maoni ya watumishi waliohudhuria mafunzo yaliofanyika kwenye ukumbi wa NEC, Makao Makuu ya CCM Ofisi Ndogo Lumumba jijini Dar es Salaam.

No comments

Powered by Blogger.