Header Ads

Wizara ya Afya yatekeleza Agizo la Rais Dkt JOHN MAGUFULI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akipokea Vitanda vya kawaida vya wagonjwa120, vya watoto njiti 10, vya kujifungulia 10, Magodoro, 120 na Shuka 480, vyote hivyo vimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kama alivyoahidi siku alipo zungumza na wazee wa mkoa wa Dar es Salaam.
Mashuka yakishushwa kwenye gari tayari kwa kupelekwa kwenye wodi mpya ambayo ilikuwa ikitumika kama ofisi hapo awali.
Magodoro yakishushwa kwenye gari kama inavyoonekana pichani.
Mafundi wakiendelea kufunga vitanda vilivyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.
Waauguzi wakitandika vitanda hivyo kama inavyoonekana.
Muuguzi akipandisha Kitanda ili kiweze kuanza kutumika.
Wagonjwa wakiwa wamelala mara baada ya kufungwa kwa vitanda hivyo.
Muuguzi akimfunika mgonjwa kama inavyoonekana mara baada ya kufungwa vitanda hivyo. 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akifanya usafi mbele ya Jengo lililokuwa Ofisi ya Wizara ya Afya ambalo kwa sasa ni Wodi mpya  ya wakina mama kama alivyoagiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. 

Picha zote  na Mpiga picha wetu

No comments

Powered by Blogger.