Header Ads

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, ANGELA KAIRUKI afanya Ziara Mkoa wa PWANI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo alipokuwa akiwasilisha taarifa ya Mkoa wa Pwani ofisini kwa Mkuu wa Mkoa huyo kabla ya kikao kazi na watumishi wa mkoa wa Pwani kilichofanyika tarehe 18/7/2016 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akiongea na watumishi wa Mkoa wa Pwani (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi na watumishi hao kilichofanyika tarehe 18/7/2016 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. 
Baadhi ya Watumishi wa Mkoa wa Pwani wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa kikao kazi na watumishi hao kilichofanyika tarehe 18/7/2016 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. 
Afisa Elimu Mkoa wa Pwani, Bw. Yusuph Kipengele akiwasilisha malalamiko yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) wakati wa kikao kazi na watumishi wa mkoa wa Pwani kilichofanyika tarehe 18/7/2016 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

No comments

Powered by Blogger.