Header Ads

Moto wateketeza Bohari Eneo la Sinza Lego Jijini Dar es Salaam

Na Fredy Njeje

Bohari moja ambalo lilikuwa la kuhifadhia mataili pamoja na vifaa vyenginevyo vya magari lililopo Sinza Lego ambalo mmiriki wake hakufahamika kwa mara moja limeteketea kwa moto ambapo kwa mujibu ya wenyeji wa eneo hilo wamedai kuwa chanzo cha moto huo ni mataili.  


Pia katika eneo hilo kuna Gereji ambayo haikuathirika na moto huo mkubwa, mpaka jioni hii kikosi cha kuzima moto kilikuwa eneo la tukio kuendelea kusaidiana na wananchi kuhakikisha moto huo unazimika. 

Taarifa kamili itatolewa na Jeshi la Polisi. Bohari likiwa linateketea kwa moto jioni hii Sinza Lego.

Mmoja wa kijana ambaye alifika kushuhudia tukio hilo akipanda juu ya Ghorofa baada ya kunusurika kudondokea katika moto huo.

Moto ukiendelea kuwaka huku juhudi za kuzima zikiendelea...

Mbele ni Gari la zima moto likiwa limefanya juhudi za kuzima moto,hapa wakiondoka kufuata maji mengine ili kuendelea na zoezi la kuzima moto huo.

Moto ukiendelea kuwaka katika Bohari hilo.

Baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia tukio hilo la kuwaka kwa Bohari.

Magari yakiwa yameruhusiwa kuendelea na safari baada ya moto huo na moshi mkubwa kupungua. 


No comments

Powered by Blogger.