Kongamano la Uwekezaji Ukanda wa Ziwa TANGANYIKA limefunguliwa
Waziri wa Nchi- Uwekezaji na
Uwezeshaji, Eng. Christopher Chiza, akizungumza kabla ya kumkaribisha
Mgeni rasmi, Makamu wa Rais Dkt. Bilal ili kufungua Kongamano hilo.
Picha zote na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati
akifungua rasmi Kongamano la Uwekezaji wa Ziwa Tanganyika, lililofanyika
leo Sept 9, 2015 kwenye Hoteli ya Tanganyika Mjini Kigoma.
Mwakilishi wa Umoja wa wafanyabishara wa Burundi, akizungumza.
Sehemu ya washiriki wa Kongamano
hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal, alipokuwa akihutubia
kwenye ufunguzi wa Kongamano hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia moja ya
jiwe lenye Madini huku akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni
ya Aifola Investiment Co. Ltd, Zubery Mabie, kuhusu upatikanaji wa
madini na utengenezaji wa Unga wa ‘Lime Powder’, wakati Makamu alipokuwa
akitembelea Mabanda ya maonesho kwenye ufunguzi wa Kongamano la
Uwekezaji wa Ziwa Tanganyika, lililofanyika leo Sept 9, 2015 kwenye
Hoteli ya Tanganyika Mjini Kigoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kutoka
kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wauza Samaki wa Mapambo, Nunu Mrisho, kuhusu
upatikanaji wa Samaki hao na soko lake , wakati Makamu alipokuwa
akitembelea Mabanda ya maonesho kwenye ufunguzi wa Kongamano la
Uwekezaji wa Ziwa Tanganyika, lililofanyika leo Sept 9, 2015 kwenye
Hoteli ya Tanganyika Mjini Kigoma.
Post a Comment