Header Ads

Kampuni ya TIGO yazindua Shindano la Wajasiriamali

 Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa shindano la Wajasiriamali ambapo ametoa wito kwa watu kushiriki ili wajiweke katika nafasi ya kushinda fedha taslimu dola za kimarekani 20,000 ambazo kila mshindi atapewa azitumie katika utekelezaji wa mawazo yao ya kibunifu.

  Meneja wa nchi wa Reach for Change, Peter Nyanda, akizungumza katika mkutano huo.
 Muhasisi wa Mfuko wa APPS and Girls, Carolyne Ekyasisiima, akizungumza jinsi mfuko huo unavyofanyakazi ya kusaidia watoto katika masomo.
 Mwanzilishi wa Shule Direct, Iku Lazaro akizungumza kwenye uzinduzi huo.
 Wanahabari wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Ni furaha tupu kwenye uzinduzi huo.
 Meneja wa Mawasiliano wa Tigo, John Wanyanja akizungumza kwenye uzinduzi huo.
 Wadau wakiwa kwenye uzinduzi.
 Mkutano wa uzinduzi huo ukiendelea.
 Madada hawa wenye fulana za uzinduzi huo wakifuatilia matukio yote kwa karibu 'Wamependeza'.
Hawa ni baadhi ya wanafunzi walionufaika na mradi huo.
Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya Simu ya Tigo kwa kushirikiana na taasisi ya Reach for Change zimezindua shindano la wajasiriamali jamii liitwalo “Tigo Digital Change-makers”lenye lengo la kuibua mawazo ya kibunifu ambayo yatasaidia kutatua matatizo yanayo wakabili watotona vijana nchini.

Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez leo ametangaza uzinduzi wa shindano hilo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo ametoa wito kwa watu kushiriki ili wajiweke katika nafasi ya kushinda fedha taslimu dola za kimarekani 20,000 ambazo kila mshindi atapewa azitumie katika utekelezaji wa mawazo yao ya kibunifu.

“Tigo ikishrikianana Reach for change itatoa tuzo ya dola za kimarekani20,000 kwa kila mmoja kwa washindi wawili ambao wataku wa na mawazo ya bunifu zaidi kiteknolojia na kidijitali yaliyo na uwezo wa kuchangia kuleta maisha bora kwa watoto katika jamii ya kitanzania,” alisema Gutierrez.

Aliongezeakwamba, “Lengo letu ni kupata mawazo ya kibunifu ya kidijitali ambayo yataleta na kutatua matatizo ya nayo wakabili watoto kwa kiwango kikubwa huku tukiendelea kuwekeza katika kukuza na kuimarisha huduma zetu za mawasiliano katika maeneo yote nchini.”

Mawazo yatakayo wasilishwa kupitia shindano hili yanatakiwa kuonyesha uwezo wa kutumia simu kidijititekinolojia ya habari na mawasiliano kuleta ufanisi wa utekelezaji wa mradi husika.
Watakaopenda kushiriki shindano hili wanaweza kutuma maombi kupitia mtandao wa www.tigo.co.tz/digitalchangemakers, kwa  mujibu wa Gutierrez.

Kwa upande wake, Meneja wa nchi wa Reach for Change, Peter Nyanda, alisema licha ya kupatakitita cha dola 20,000 washindipia watapewa vifaa vya kuendeleza utekelezaji wa mawazo yao ikiwa ni pamoja na kupata ushauri kutoka kwa wafanyakazi waandamizi kutoka Tigo na Reach for Change.

Aidha wata unganishwa na wajasiriamali wengine ambao tayari wamenufaika kutokana na mpangohuo.

Mchakato huu wa kuwapata wajasiriamali jamii wakidigitali unaendana na mkakati waTigo wa kuendeleza maisha ya kidijitalinchini.

Huu ni mwaka wa nne mfululizo ambapo taasisizaTigo na Reach for Change zimekuwazikishirikiana kuwasaidia wajasiriamali nchini. Jumla ya wajasiriamali watano wa menufaika na mpango katika kipindi hiki ambao kwapamoja na kupitia utekelezaji wa miradi yao wamewasaidia jumla ya watoto zaidi ya 10,000 nchini.

No comments

Powered by Blogger.