Header Ads

Mgombea Urais wa Zanzibar CUF, Maalim SEIF SHARIF HAMAD, akutana na Jumuiya ya Akina Mama wa Chama hicho

Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na timu za ushindi za wanawake (CUF) kwa upande wa Unguja, wakati akizizindua rasmi kwenye ukumbi wa Majid Kiembe samaki.
Baadhi ya wajumbe wa Timu za ushindi za wanawake wa CUF Unguja, wakifuatilia mkutano huo.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Nassor Ahmed Mazrui, akizungumza na timu za ushindi za wanawake (CUF) kwa upande wa Unguja, wakati akizizindua rasmi kwenye ukumbi wa Majid Kiembe samaki.
Na: Hassan Hamad (OMKR)
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, ameipongeza Jumuiya ya akinamama wa Chama hicho kwa mwamko wanaouonesha katika kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu.
 
Amesema hali hiyo ni dalili njema ya mafanikio kwa chama hicho, kwa vile wanawake ambao wanachukua asilimia kubwa ya wapiga kura wa Zanzibar, wanaonekana kuwa mstari wa mbele kwenye kampeni za uchaguzi katika ngazi zote.
 
Maalim Seif ambaye pia ni mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, ametoa kauli hiyo wakati akizindua timu za ushindi za wanawake wa CUF kwa upande wa Unguja, katika mkutano maalum uliofanyika ukumbi wa Majid, Kiembesamaki.
 
Amewataka wanawake hao kufanya kazi ya ziada ili kuhakikisha kuwa Chama Cha Mapinduzi kinaondoka madarakani katika uchaguzi mkuu ujao.

No comments

Powered by Blogger.