Header Ads

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, SAID MECK SADICK AONGOZA ZOEZI LA KUOSHA MAGARI, LA MEDIA CAR WASH FOR CANCER

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadick akizindua zoezi la kuosha Magari katika viwanja vya Leaders Club kwa ajili ya kuchangia Fedha kwa waandishi wa Habari ambao wanamatatizo ya Kiafya ikiwemo Saratani. 

 Mkuu wa Wilaya ya Kinomdoni Paul Makonda Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kuongea na Waandishi wa Habari pamoja na wadau. 

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadick akiongea na waandishi wa Habari pamoja na Wadau mbalimbali waliofika kuosha Magari yao kwa ajili ya kuwachangia waandishi wa Habari wenye Matatizo ya Saratani.
 Wakielekea kuosha Magari.
Mkurugenzi Mkuu wa Habari Maelezo(wa kwanza kushoto)  Athur Mwambene Akiosha Gari.
 Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe akiosha Gari wakati wa  Shughuli hiyo maalum kwa ajili ya Kuchangia waandishi wenye udhoofu wa afya zao.
Mzee wa Father Kidevu Blog  Ambaye pia ni mwana TBN  akiendelea na yake....
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akiosha Pikipiki wakati wa shughuli hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akiendelea Kuosha moja ya Magari yaliyofika kuoshwa katika Media Car Wash for Cancer. Ikiwa ni kuchangia waandishi wa habari wenye magonjwa mbalimbali ikiwemo Saratani.
Ankali Issa Michuzi wa Libeneke la Michuzi Blog na Michuzi Media Group na Mwana TBN  akiwa Bizeee... Anaosha Moja ya Magari kwa ajili ya kuchangia waandishi wa habari ambao wanamaradhi ya Saratani.
 Watu wanazidi kuchangia .....
Hapa ni zaidi ya Tsh 1,600,000 zimechangishwa na kukabidhiwa.
 
Chezea Changizo wewe.
 Waandishi wakichukua kwa Makini Tukio zima.
Picha ya pamoja ya waandishi wa Habari pamoja na Baadhi ya Viongozi.

Unaweza Changia pia kupitia M-Pesa 0766 970240
au
Tigo Pesa 0653 155 808

(Picha zote na Fredy Tony Njeje wa Blogs za Mikoa.)

No comments

Powered by Blogger.