Waziri waNchi, Ofisi ya Makamuwa Rais,
Muungano na Mazingira Mh. January
Yusuph Makamba akiongea na wataalamu wa Mazingira katika Mkutano waTatu wa Chama cha
Wataalam wa Tathmini ya Athari za Mazingira jijini Dar es Salaam. ..................................
Na: Frank Shija –
MAELEZO
Wataalamu wa Tathmini
ya Athari za Mazingira nchini wametahadharishwa kuwepo kwa matapeli wanaingilia
taaluma hiyo kwa lengo la kufanya udanganyifu na kujipatia kipato.
Hayo yamesemwa leo na
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira January Makamba
wakati akifungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Tathmini ya
Athari za Mazingira Tanzania (TEEA) leo Jijini Dar es Saalam.
Makamba amesema kuwa
taaluma ya tathmini ya Athari za Mazingira ni ya shughuli ambayo inahitaji
mkubwa sana na ni kwa mujibu wa sheria za nchi lakini kumekuwapo na makanjanja
ambao wamekuwa wakifanya uraghai kwa wawekezaji na kutia doa tasnia nzima ya
taaluma ya uthamini wa athari za mazingira.
“Serikali inakusudia
kubadilisha kanuni na taratibu ili kuongeza udhibiti wa udanganyifu katika eneo
la Tathmini ya Athari za Mazingira(IAE) kwa kuweka viwango stahiki kwa
wataalamu wa tathmini ya athari za mazingira vitakavyozingatia elimu na
uzoefu,” alisema Makamba.
Aliongeza kuwa ni
vyema sasa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na
Chama cha Wataalumu hao kushirikiana kuhakikisha taaluma hiyo haingiliwi na makanjanja
ili kufanikisha utoaji wa huduma zenye viwango stahiki na vya kuridhisha.
Awali akiwasilisha
salamu za Bodi ya Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Profesa
Ruben Mwamakimbullah amesema amemshukuru Waziri Makamba kwa kukubali kujumuika
na wataalamu hao katika mkutano huo muhimu na kuongeza kuwa wao kama Bodi
watafanyia kazi ushauri wote alioutoa na kuahidi kuongeza ufanisi katika
kutekeleza majukumu yao ili kuleta heshi kwa tasnia ya tathmini ya athari za
mazingira na taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mhandisi
Bonaventure Baya amesema kuwa mkutano huo umekuwa ukiwakutanisha Wataalamu wa
Tathmini ya Athari za Mazingira nchini ambapo utumia fursa hiyo kukumbushana
mambo yanayohusu weledi na majukumu yao.
Mkurugenzi huyo
amesema kuwa mkutano huo ni wa tatu kufanyika ambapo umetanguliwa na mikutano
iliyofanyika februari 2011 na Machi 2015
na kuongeza kuwa NEMC imekuwa ikiratibu mkutano huo kwa lengo la kuwakutanisha
Wataalamu wa Tathmini ya Athari za Mazingira nchini ili kujadili changamoto zao
na kupeana uzoefu.
|
Post a Comment