Header Ads

Serikali yawatahadharisha Watalaamu wa Athari za Mazingira Kuhusu Uwepo wa Vishoka


Waziri waNchi, Ofisi ya Makamuwa Rais, Muungano na Mazingira Mh. January Yusuph Makamba akiongea na wataalamu wa Mazingira katika Mkutano waTatu wa Chama cha Wataalam wa Tathmini ya Athari za Mazingira jijini Dar es Salaam.
..................................
Na: Frank Shija – MAELEZO

Wataalamu wa Tathmini ya Athari za Mazingira nchini wametahadharishwa kuwepo kwa matapeli wanaingilia taaluma hiyo kwa lengo la kufanya udanganyifu na kujipatia kipato.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira January Makamba wakati akifungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Tathmini ya Athari za Mazingira Tanzania (TEEA) leo Jijini Dar es Saalam.

Makamba amesema kuwa taaluma ya tathmini ya Athari za Mazingira ni ya shughuli ambayo inahitaji mkubwa sana na ni kwa mujibu wa sheria za nchi lakini kumekuwapo na makanjanja ambao wamekuwa wakifanya uraghai kwa wawekezaji na kutia doa tasnia nzima ya taaluma ya uthamini wa athari za mazingira.

“Serikali inakusudia kubadilisha kanuni na taratibu ili kuongeza udhibiti wa udanganyifu katika eneo la Tathmini ya Athari za Mazingira(IAE) kwa kuweka viwango stahiki kwa wataalamu wa tathmini ya athari za mazingira vitakavyozingatia elimu na uzoefu,” alisema Makamba.

Aliongeza kuwa ni vyema sasa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Chama cha Wataalumu hao kushirikiana  kuhakikisha taaluma hiyo haingiliwi na makanjanja ili kufanikisha utoaji wa huduma zenye viwango stahiki na vya kuridhisha.

Awali akiwasilisha salamu za Bodi ya Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Profesa Ruben Mwamakimbullah amesema amemshukuru Waziri Makamba kwa kukubali kujumuika na wataalamu hao katika mkutano huo muhimu na kuongeza kuwa wao kama Bodi watafanyia kazi ushauri wote alioutoa na kuahidi kuongeza ufanisi katika kutekeleza majukumu yao ili kuleta heshi kwa tasnia ya tathmini ya athari za mazingira na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mhandisi Bonaventure Baya amesema kuwa mkutano huo umekuwa ukiwakutanisha Wataalamu wa Tathmini ya Athari za Mazingira nchini ambapo utumia fursa hiyo kukumbushana mambo yanayohusu weledi na majukumu yao.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa mkutano huo ni wa tatu kufanyika ambapo umetanguliwa na mikutano iliyofanyika  februari 2011 na Machi 2015 na kuongeza kuwa NEMC imekuwa ikiratibu mkutano huo kwa lengo la kuwakutanisha Wataalamu wa Tathmini ya Athari za Mazingira nchini ili kujadili changamoto zao na kupeana uzoefu.

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mwandisi Bonaventure Baya akiongea na wataalamu wa Mazingira katika Mkutano wa Tatu wa Chama cha Wataalam wa Tathmini ya Athari za Mazingira nchini Dar es Salaam. 

Mjumbe wa Bodi wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Prof. Ruben Mwamakimbullah akitoa salamu za Bodi kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya Mazingira Prof. Salome Misana katika Mkutano wa Tatu wa Chama cha Wataalam wa Tathmini ya Athari za Mazingira Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mh. January Yusuph Makamba akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa Mazingira katika Mkutano wa Tatu wa Chama cha Wataalam wa Tathmini ya Athari za Mazingira Jijini Dar es Salaam.

(Picha zote na Benjamin Sawe)

No comments

Powered by Blogger.