Mkurugenzi Mkuu wa
Kampuni Hodhi Miliki ya Rasilimali za Reli (RAHCO), Masanja Kadogosa (wa tatu
kutoka kulia), akibadilishana Mkataba wa awamu ya kwanza ya ujenzi wa reli ya
Kisasa (Standard Gauge), na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mota-Engil
Africa, Bw. Manuel Antonio Mota, mara baada ya kusaini mkataba huo jijini Dar
es Salaam.
..........................................
Serikali imetiliana
saini ya makubaliano ya ujenzi wa sehemu ya kipande cha reli ya kisasa
(Standard Gauge), chenye urefu wa KM 300 kati ya mkoa wa Dar es Salaam na
Morogoro ambao ujenzi wake unatarajiwa kuanza baada ya mwezi mmoja na nusu
kutoka sasa.
Kampuni zilizotiliana
saini makubaliano hayo na Serikali ni ya ubia kati ya YAPI MERKEZI ya uturuki na MOTA-ENGIL
AFRIKA ya ureno kwa grahama ya dola zaidi ya bilioni moja za kimarekani.
Akishuhudia utiliaji
saini uliofanyika jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema ujenzi wa reli hiyo itayotumia umeme
na kwenda kwa spidi ya kilometa 160 kwa saa itakuwa ni ya kwanza kwa Afrika
ikifuatiwa na nchi ya Morocco.
“Tunataka kuifanya
nchi yetu iwe ndogo kwa kutumia miundombinu ya kisasa ndio maana Serikali
imeamua kujenga reli hii itakayotumia umeme na kwenda spidi kubwa kuliko
nyingine zote barani Afrika”, amesema Prof. Mbarawa.
Ameongeza kuwa ujenzi
wa reli hiyo utaongeza chachu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi
na kubainisha kuwa Safari ya Dar hadi Moro itatumia muda wa saa 1:16 wakati Dar
hadi Dodoma itatumia muda wa saa 2:30 na safari ya Dar had Mwanza itatumia muda
wa saa 7:30.
Aidha, Prof. Mbarawa
amesisitiza kuwa gharama za ujenzi wa reli hiyo haitakuwa sawa na mikoa mingine
kutokana na kutofautiana na hali ya jiografiia kwenye mikoa ambapo reli hiyo
itapita.
Kuhusu kukamilisha
mradi huu, Waziri Prof. Mbarawa ameahidi kuongeza bajeti ya ujenzi wa reli hiyo
kwa mwaka ujao wa fedha na kuendelea kutafuta mkopo wa gharama nafuu ili
kufanikisha ukamilishawaji wake.
Waziri Prof. Mbarawa
amewataka wadau kujitokeza kwa wingi kuomba zabuni zIlizotangazwa hivi karibuni
za ujenzi wa reli hiyo kwa awamu nyingine kutoka Morogoro-Makotopora KM 336,
Makotopora-Tabora KM 294, Tabora-Isaka KM 133 na Isaka hadi Mwanza KM 248 ambazo
zinatarajiwa kufunguliwa mwezi Aprili mwaka huu na kuahidi kuwa utaratibu wake
utatendeka kwa uwazi na haki.
Naye Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni Hodhi Miliki ya
Rasilimali za Reli (RAHCO), Masanja Kadogosa amesema kuwa ujenzi wa reli hiyo utajengwa
kwa muda wa miezi 30 kutokea sasa na kuhusisha
ujenzi wa miundombinu ya umeme, Stesheni sita za abiria na sita za kupishani
treni na ujenzi wa wigo wa KM 102 kwa usalama wa watu na magari.
Kwa upande wake Balozi
wa Uturuki nchini Mhe. Yassemin Eralp ameiahidi kuendeleza ushirikiano na Serikali
katika mradi huo mkubwa na kuupongeza uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano
katika kufanikisha maendeleo kwa wananchi wake.
|
Post a Comment