Header Ads

Watumishi Wizara ya Ardhi Washiriki Bonanza la Michezo ya SHIMIWI Jijini Dar es Salaam

Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, leo wameshiriki katika Bonanza Maalumu la Michezo ya SHIMIWI kwa watumishi wa Umma, ambalo limefanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.

Katika Bonanza la leo Mgeni rasmi alikuwa ni Katibu mkuu Utumishi, akimwakilisha Katibu mkuu Kiongozi Balozi JOHN KIJAZI.


Watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambao wameshiriki Bonanza la Michezo ya SHIMIWI liliofanyika leo kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, wakiwa wamepozi katika Picha ya pamoja. 
Waliosimama Kutoka Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Dkt Kusiluka, Mkurugenzi wa ICT Eliasi Nyabusani pamoja na Msajili wa Hati Subira Sinda wakibadilishana Mawazo leo wakati wa Bonanza la Michezo la SHIMIWI kwa watumishi wa Umma  lililofanyika katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa ICT Eliasi Nyabusani ( katikati ) na Mwenyekiti wa Michezo wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ndugu Swagile Msananga wakiwa Sambamba na Katibu ndugu Mwikari Mshana wakati wa Bonanza la Michezo ya SHIMIWI lililofanyika leo Jijini Dar es Salaam Kwenye Uwanja wa Uhuru.

No comments

Powered by Blogger.