Header Ads

Kishindo cha tiGO FIESTA 2016 chatikisa Jiji la TANGA

Roma Mkatolili akitumbuiza katika jukwaa la Tigo Fiesta katika Tamasha hilo liliofanyika katika viwanja vya  Mkwakwani Jijini Tanga usiku wa Ijumaa .
Nahreel na Aika toka Kundi la Navykenzo wakilishambulia jukwaa la Tigo Fiesta katika viwanja vya Mkwakani Jijini Tanga.
Shetta akiwa na wacheza wake akitoa burudani kwa maelf ya mashabiki waliojitokeza  katika Viwanja vya Mkwakwani usiku wa Ijumaa. 
Kundi la weusi wakitoa burudani na michano ya nyimbo zao kali kwa wapenzi wa muziki waliojitokeza katika Tamasha la burudani la Tigo Fiesta jijini Tanga.
 Barnaba akiwa  kwenye  jukwaa la Tigo fiesta uwanja  wa  Mkwakwani   Tanga  usiku  wa  ijumaa hii.
Benpol akitumbuiza kwa Style ya Mduara na wacheza shoo wake. 
DOGO JANJA naye akiwakonga wapenzi wa muziki waliojitokeza katika Tamasha la Tigo fiesta.
Makomandoo wakionesha umahiri wao wa kumiliki jukwaa. 
Maua Sama naye aliwakonga nyoyo wapenzi wa burudani waliojitokeza kwa wingi katika Tamasha la Tigo Fiesta jijini Tanga.
Nay wa Mitego akilivamia jukwaaa la Tigo Fiesta katika Tamasha hilo lililofanyika katika viwanja vya Mkwakani usiku wa ijumaa wiki hii.
Maelfu ya wakazi wa jiji Tanga waliojitokeza katika viwanja vya Mkwakwani katika Tamasha la Tigo Fiesta wakipata burudani kwa wasanii wa Bongofleva na Vikundi vya Taarabu vilivyotoa burudani ya kukata na shoka usiku  wa ijumaa.

No comments

Powered by Blogger.