Header Ads

Semina ya Mchezo wa KARATE yaanza Jijini Dar es Salaam

Senpai Esther Thomas (kushoto) akipangua chudan tzuki (ngumi ya kifua) wakati semina hiyo ikiendelea.

Anafundisha kwa mifano! Shihan Okuma akishambuliwa na Jerome Sensei kama sehemu ya maelekezo katika semina hiyo

Na Daniel Mbega


SEMINA kubwa ya Shotokan Karate kwa nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini, imeanza leo hii jijini Dar es Salaam ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya mchezo huo nchini Tanzania, inaongozwa na mkufunzi mkuu, Shihan Koichiro Okuma (6th Dan), kutoka makao makuu ya chama cha karate cha Japan Karate Association/World Federation (JKA/WF), Tokyo, Japan.

Semina hiyo – maarufu kama JKA/WF- Tanzania Southern, Central & East African Region Gasshuku – ambayo imeandaliwa na chama cha Japan Karate Association/World Federation-Tanzania (JKA/WF-Tanzania) ni ya nane kufanyika ambapo kwa mwaka huu inashirikisha makarateka 45 kutoka Zimbabwe, Zambia, Uganda, Kenya na wenyeji Tanzania.

Kwa mujibu wa JKA/WF-Tanzania, semina hiyo ya wiki nzima inatarajiwa kufikia tamati Jumamosi.


Makarateka ambao wameanza kushiriki leo hii, kutoka Tanzania ni Jerome Mhagama Sensei, Justine Limwagu, Seberian Dagila, Said O. Kissailo, Lulangalila Lyimma, Athumani Kambi, Mikidadi Kilindo Sensei, Marcus George, Khamis K. Sambuki, Hamis Said Mkumbi, Selemani A. Mkalola, Christopher William, Eliasa Mohammed, Adson Aroko Sensei, Nestory Federicko, Daniel Mbega, Willy Ringo Rwezaura Sensei, na Shihan Dudley Mawala Sensei, ambaye alikuwa mgeni mwalikwa.


Makarateka wengine na nchi zao kwenya mabano ni Gibson Sangweni (Zimbabwe), Robert Chisanga (Zambia), Thobias B. Rudhal (Kenya), George Otieno (Kenya), Joshua Oude (Kenya), George Warambo (Kenya), George Okeyo (Kenya), Florence Kieti (Kenya), Asana Mahmoud Ulwona (Uganda), Ofubo Issa Yahaya (Uganda), Magezi Yasiin (Uganda), Wanyika Abdurahman (Uganda), Frederic Kilcher (Ufaransa) na Koichiro Okuma (Japan).


Mkufunzi mkuu wa JKA/WF-Tanzania, Jerome George Mhagama Sensei (5th Dan), amesema hata hivyo kwamba, tofauti na miaka iliyotangulia, safari hii hakutakuwa na mashindano ili kutoa fursa kubwa kwa Shihan Okuma kufundisha vyema na kuwapandisha madaraja makarateka mbalimbali kuanzia ngazi ya Sho-Dan, Ni-Dan, San-Dan na Yon-Dan (1st – 4th Dan).



 Shihan Okuma akitoa neno kabla ya kuanza kwa semina leo hii mchana.

 Shihan Okuma akijiandaa kuanza darasa leo mchana. Kushoro ni Willy Ringo Rwezaura Sensei.

 Timu ya Kenya hii.

 Makarateka wanapasha misuli.

 Heian Shodan Kata.

No comments

Powered by Blogger.