Header Ads

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani PROJEST RWEGASIRA azungumza na Wakuu wa Vitengo

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, akizungumza na wakuu wa Idara na vitengo  vilivyopo chini ya wizara  wakati wa mkutano wa kujadili masuala ya kiutendaji katika wizara hiyo, Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya.Mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Wakuu wa Idara na Vitengo wa  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira, wakati wa mkutano wa kujadili masuala  ya kiutendaji katika wizara  hiyo, Mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Viongozi kutoka Idara za Wizara ya Mambo ya Ndani, kutoka kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Minja, Kamishna wa Operesheni Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Rogasius Kipali na Kamishna wa Fedha Jeshi la Polisi, Albert Nyamhanga, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa wizara, Meja Jenerali Projest Rwegasira(hayupo pichani) wakati wa mkutano wa kujadili masuala  ya kiutendaji katika wizara hiyo. Mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam.

No comments

Powered by Blogger.