Header Ads

Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyama Pori ( JUHIWANGUMWA ) yatambuliwa Kisheria

        Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen Gaudence Milanzi akizungumza kwenye  mkutano  kabla ya  kukabidhi  rasmi hati mbili kwa pamoja    ya kuitambua Jumuiya ya JUHIWANGUMWA  kama chombo halali kilichosajiliwa kisheria kwa ajili ya  kusimamia rasilimali za wanyamapori zilizopo ndani ya eneo laJumuiya hiyo kwa tangazo la serikali  Na. 204 na hati ya matumizi endelevu ya rasilimali za Maliasili. Makabidhiano hayo yamefanyika  jana   katika kijiji cha Utete Wilayani Rufiji 
        Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen Gaudence Milanzi  akikabidhi  rasmi hati  kwa kiongozi wa  Jumuiya ya Uhifadhi wa Wanyamapori  ya  JUHIWANGUMWA Bw. Shaban Dinongo ya kuitambua Jumuiya hiyo  kama chombo halali kilichosajiliwa kisheria kwa ajili ya  kusimamia rasilimali za wanyamapori zilizopo ndani ya eneo laJumuiya hiyo kwa tangazo la serikali  Na. 204. Makabidhiano hayo yamefanyika jana  katika kijiji cha Utete Wilayani Rufiji

.................

Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen Gaudence Milanzi,  imekabidhi  rasmi hati ya  ya kuitambua Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya  JUHIWANGUMWA  kama chombo halali kilichosajiliwa kisheria kwa ajili ya  kusimamia rasilimali za wanyamapori zilizopo ndani ya eneo  la Jumuiya hiyo, Rufiji mkoani Pwani.

Pia, imekabidhi hati ya matumizi endelevu ya rasilimali za Maliasili hususani wanyamapori  kwa kuwapa wananchi  mamlaka ya kusimamia na kutumia rasilimali hizo  kwa kuwa na uhifadhi na maendeleo endelevu kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho katika maeneo yao, Taifa na Dunia kwa ujumla. 

Akizungumza jana  katika kijiji cha Utete wilayani  Rufiji  wakati  akikabidhi  hati hizo mbili kwa  pamoja kwa Jumuiya ya hifadhi ya wanyamapori ya JUHIWANGUMWA , Milanzi amewatahadhalisha  Viongozi wa Jumuiya  hiyo  kuwa na  waadilifu  wawazi  hususani  katika  masuala ya pesa na mikataba watakayoingia na wawekezaji ili kuweza kuepuka migogoro isiyo ya lazima kutoka kwa Wananchi  ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara  katika jumuiya nyingine.

‘’Tunataka fedha  zitakazopatikana  kupitia   utalii wa Picha  na utalii wa uwindaji    ( photographic and tourist hunting) zitumike katika huduma za kijamii kwa kuboresha  miundombinu, shule, hospitali na huduma nyinginezo za kijamii na sio pesa hizo zitumike kuwaneemesha watu wachache’’ alisema Milanzi

Aliongeza kuwa, Serikali kuu ( Wizara) itaendelea kuwasaidia pale inapohitajika kufanya hivyo katika masuala ya Uhifadhi,  ‘’hatutaki  kuwaingilia katika masuala yenu mfano  katika   masuala ya mapato na matumizi hivyo  nawataka mshirikiane na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya  ili msiweze kutumbukia kwenye migogoro ya namna hiyo’’ alisisitiza Milanzi

Aidha , Maj.Gen. Milanzi amewataka Wakuu wa  Wilaya ya Rufiji,  Malinyi, Kilombero na  Ulanga ambazo ni Wilaya  zinazounda jumuiya hiyo ya JUHIWANGUMWA  yenye ukubwa wa kilomita za mraba 496.5 Kuhakikisha kuwa wanashirikiana na wananchi   kuzuia mifugo isiingie  ndani ya hifadhi kwa kuwa ni kinyume cha sheria ya uhifadhi kulisha mifugo hifadhini.

Milanzi alisema ‘’ Suala la kuingiza mifugo kwenye hifadhi lisiwe  la kisiasa ni lazima kila mwananchi atambue kuingiza mifugo ndani ya hifadhi ya wanyamapori ni kuvunja sheria ya Uhifadhi hivyo atakayebainika lazima sheria ifuate mkondo wake’’

No comments

Powered by Blogger.