Taasisi za Elimu zaombwa Kuwathamini Wahitimu waliofanya Vizuri
![]()  | 
| Wageni mbalimbali wakitembelea eneo la Vipimo na Mizani wakati wa hafla ya utoaji wa Tuzo na zawadi kwa wahitimu waliofanya vizuri katika masomo yao katika Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es salaam. | 
![]()  | 
| Baadhi ya wanafunzi na wahitimu wakitembelea mabanda ya maonesho. | 
![]()  | 
| Mmoja wa Wahitimu wa CBE aliyefanya vizuri katika fani ya Rasilimali Watu Bi. Happyness Onani akipokea cheti kutoka kwa Mkuu wa Chuo hicho Prof.Emmanuel Mjema. | 
Baadhi ya wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya utoaji wa Zawadi na kwa wahitimu iliyofanyika CBE kampasi ya Dar es Salaam.
Na Aron Msigwa - MAELEZO
Taasisi
 za elimu kote nchini zimeaswa kujenga utamaduni wa kuthamini na 
kutambua mchango wa wahitimu wanaofanya vizuri katika masomo yao 
Hayo
 yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa Chuo cha Elimu ya 
Biashara Dar es Salaam (CBE) Prof.Emanuel Mjema wakati wa hafla ya 
kuwatunuku vyeti na zawadi mbalimbali wahitimu wa chuo hicho takribani 
20  waliofanya vizuri katika masomo yao kwa mwaka 2015.
Akizungumza
 na jamii ya wanachuo na Wahitimu wa Zamani wa Chuo cha Elimu ya 
Biashara na wale wanaofanya kazi katika maeneo mbalimbali nchini amesema
 chuo chake kina utamaduni wa kuwatuza wahitimu wanaofanya vizuri katika
 masomo yao kama  motisha kuthamini juhudi zao ili kuhamasisha wengine 
kufanya vizuri zaidi.
Amesema wahitimu 20 wa 
fani mbalimbali zikiwemo za Rasilimali Watu,Uendeshaji wa Biashara, 
Ununuzi na Ugavi, Vipimo na Mizani, Uhasibu, Ununuzi na Ugavi,  Masoko 
na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ngazi ya Stashahada, 
Shahada,Diploma  na Cheti wametunukiwa vyeti na kukabidhiwa zawadi 
mbalimbali.
Prof. Mjema ameongeza kuwa mbali na
 tuzo hizo wadau hao hususan wahitimu wa miaka ya nyuma wa chuo hicho 
wapata fursa ya kujadili masuala mbalimbali ikiwemo kukijengea uwezo 
chuo hicho pamoja na  kuangalia shughuli za kitaaluma  zinazofanyika.
"
 Siku hii ni muhimu sana kwa Chuo cha Elimu ya Biashara, ni siku ambayo 
tunathamini wahitimu wetu waliofanya vizuri kwa  kuwapa  Zawadi za vtu 
mbalimbali kuthamini mchango na heshima waliokipa chuo chuo chetu" 
Alisisitiza Prof.Mjema.
Ameongeza kuwa utoaji 
wa zawadi na tuzo hizo unakwenda sambamba na na maadhimisho ya ya 
Mahafali ya 50 ya chuo hicho kampasi ya Dar es Salaam yatakayofanyika 
Novemba 12,2015 katika ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo mgeni rasmi 
atakua Rais mstaafu wa awamu ya Pili  Ali Hasani Mwinyi.
Akifafanua
 kuhusu mahafali hayo ya 50 amesema kuwa wahitimu wapatao 2050  wa ngazi
 mbalimbali watatunukiwa Shahada , Astashahada, Stashahada, shahada na 
stashahada za Uzamili. 
Kuhusu suala la nidhamu
  chuoni hapo hasa mavazi amesema kuwa chuo chake kimeendelea kusisitiza
 nidhamu na kuweka kanuni zinazowabana wanafunzi huku akifafanua kuwa 
chuo hicho kilikua chuo cha kwanza kuweka sheria inayosimamia nidhamu ya
 mavazi kwa wanafunzi.
Amesisitiza kuwa mavazi 
ndiyo yanayompambanua mwananfunzi na kuonyesha tabia yake na kuongeza 
kuwa nidhamu inapokua juu inawapa wanafunzi fursa nzuri ya kupata ajira 
pindi wanapohitimu kwa kuwa tayari wanaaminika katika jamii.
Prof.Mjema
 amebainisha hali ya nidhamu ya mavazi inaendelea kuzingatiwa kutokana 
na Madhara ya kuzuiwanna kushindwa kuhudhuria vipindi wanayoyapata 
wanafunzi waliokuwa wanakiuka kanuni na taratibu za chuo hicho 
"Vijana
 lazima wawe mfano wa kuiga na hawa ni wasomi ambao wanategemewa na 
taifa, CBE imeshafukuza wengi kwa kukosa nidhamu, pia mwanafunzi 
anayekosa maadili huathiri maendeleo ya chuo na wanafunzi wengine" 
Amesisitiza.
Akizungumza kwa niaba ya wahitimu 
wa zamani wa chuo hicho (Alumnae) Bw.Lusekelo Mwandemange  amesema kuwa 
wao kama wahitimu wanayo dhamana   ya kuhakikisha maendeleo ya chuo 
hicho yanapatikana.
Amesema wahitimu hao 
wamekuwa kioo kwa jamii inayowazunguka kwa kuitumia elimu yao kutatua 
changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii
Aidha
 wameupongeza uongozi wa chuo hicho kwa kuendelea kuweka mazingira 
rafiki ya kuwawezesha wanafunzi wa chuo hicho katika fani mbalimbali 
kupata elimu yenye viwango ndani na nje ya nchi.
Pia wamesema kuwa wao kama wahitimu wameanzisha umoja wao utakaohusika kuchangia maendeleo ya chuo hicho.






Post a Comment