Header Ads

KATIBU MKUU WA CCM NDG, ABDULRAHMAN KINANA NA UJUMBE WAKE WATEMBELEA VISIWA VINNE WILAYANI MULEBA MKOANI KAGERA

Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana,  akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Mpira, mjini Muleba mkoani Kagera.Ndugu Kinana yuko katika ziara ya siku kumi mkoani Kagera ya kuimarisha na kukagua utekelezwaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2010,ikiwemo pia kusikiliza matatizo ya wananchi na kuyatafutia ufumbuzi.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, akihutubia wananchi katika  mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Mpira wa Muleba mjini mkoani Kagera.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwa pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wananchi (hawapo pichani),walipokuwa wakiwasili kwa boti katika kisiwa cha Iroba-Bumbile,wilayani Muleba.

 
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwapungia mkono wananchi alipowasili kwa mtumbwi katika kijiji cha Katunguru, baada ya kutembelea visiwa zaidi ya vinne, katika wilaya ya Muleba,kulia kwake ni Prof Tibaijuka ambaye ni Mbunge wa jimbo la Muleba kusini,Kinana yuko kwenye ziara ya siku kumi kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, na uhai wa Chama katika wilaya hiyo mkoani Kagera.

 

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasili kwenye Kisiwa cha Iroba-Bumbile wilayani Muleba mkoani kagera.

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwa  na Mbunge wa jimbo la Muleba Kusini Mh. Profesa Anna Tibaijuka wakijadiliana jambo katika boti wakati wakijiandaa kusafiri kwenda kisiwa cha Iroba-Bumbile,wilayani humo mkoani Kagera.

 

Sehemu ya umati wa watu wakiwa kwenye mkutano huo wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana mjini Muleba mkoani Kagera .

PICHA NA MICHUZI JR-MULEBA-KAGERA.

KUONA PICHA ZAIDI  BOFYA HAPA

au

HAPA

No comments

Powered by Blogger.