Header Ads

KOMREDI ABDULRAHMAN KINANA, AZUNGUMZA NA WANANCHI WA WILAYA YA KWIMBA JIJINI MWANZA

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Ngudu kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Ngudu mjini wilayani Kwimba.

 Umati wa wakazi wa Ngudu wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa akihutubia kwenye uwanja wa michezo Ngudu wilayani Kwimba.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Ngudu mjini ambapo kupitia mkutano huo alitoa msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kulaani mauaji ya Albino na Vikongwe na kutaka mabalozi wa nyumba kumi wasaidie kuwapata wahusika.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati akihutubia wakazi wa mji mdogo wa Ngudu wilayani Kwimba.

 Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu akisalimu wananchi wa mji mdogo wa Ngudu na kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM mkoa.

 Diwani wa kata ya Ngudu Faisal Mohamed akihutubia kwenye mkutano wa hadhara amabapo alieleza mafanikio ya kata yake katika kutekeleza ilani ya Uchaguzi mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

 Wananchi wakifuatilia kwa makini hotuba za viongozi wao.

 Mbunge wa Jimbo la Kwimba Shanif Mansoor akihutubia wakazi wa Ngudu mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara ambao mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

 Uwanja wa Ngudu ukiwa umefurika na wananchi waliokuja kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahma Kinana ambaye ameongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa jukwaani na baadhi wa wakazi wa kata ya Ngudu walioamua kurejea CCM kutoka upinzani.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma bango wakati wa mapokezi kwenye mradi wa Umoja wa vijanaMazingira Ngudu.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. Magessa Mulongo kwenye mradi wa vijana wa kuotesha miche.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa mradi wa umoja wa vijana wa kuotesha miche Ngudu,wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda mbegu za miche ya miti kwenye mradi wa Vijana Mazingira Ngudu wilayani Kwimba.

 Diwani wa kata ya Ngudu Faisal Mohamed akitoa maelezo ya mradi wa maji kwenye Kata ya Ngudu ambao utanufaisha zaidi ya wakazi 51,000.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji Bi. georgina Jacob mkazi wa Kakora Ngudu .

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka kuona na kukagua wodi daraja la pili  kwenye hospitali ya Wilaya ya Ngudu ambapo alipata fursa ya kutembelea jengo la wagonjwa mahututi.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman kinana akisamiliana na Balozi wa Shina namba 12 Ngudu, Bi. Specioza Balele.
Katibu Mkuu wa CCM ameweka utaratibu wa kuwatembelea mabalozi wa mashina na kuwataka viongozi wengine waige mfano.

 Mkuu wa Wilaya ya Kwimba akisalimia wananchi wa shina namba 12 kwa Balozi Specioza Balele wa Ngudu.

 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Magessa Mulongo akiwasalimu wakazi shina namba 12 kwa Balozi Specioza Balele.

Balozi wa shina namba 12 Bi.Specioza Balele akiwasalmia wananchi wake kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Andulrahman Kinana.
(Picha zote na Adam Mzee)

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments

Powered by Blogger.