Header Ads

Wadau wa Korosho Wazitaka Halmashauri Kutenga Maeneo ya Viwanda

Kikao cha wadau wa zao la korosho kimezitaka halmashari za mikoa Mitano inayolima zao hilo kutenga maeneo ya ujenzi wa viwanda pamoja na kuingia ubia na sekta binafsi.

Hiyo ni Katika kuunga mkono sera za serikali ya awamu ya Tano inayotaka kuwa na Tanzania yenye Viwanda.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho kilichohudhuriwa na wakuu wa mikoa Mitano inayolima korosho nchini, mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela, amesema namna bora ya kuboresha soko la zao hilo ni kuwa na viwanda vya kutosha vya kubangua korosho.

Rajabu Ng'onoma na Yusufu Nanila ni Wenyeviti wa vyama vikuu vya Ushirika kutoka katika mikoa ya Pwani na Mtwara wameeleza azma yao juu ya ujenzi wa maghala ya kuhifadhia korosho, huku wakiiomba Bodi ya Korosho Nchini CBT kufanya Jitihada za ujenzi wa viwanda.

Kikao hicho kilichowakutanisha wadau wa zao la korosho ikiwa ni pamoja na wakuu wa mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Ruvuma na Tanga kimejadili mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika uendeshaji wa msimu wa korosho nchini kwa mwaka 2016/2017.

No comments

Powered by Blogger.