MTV EMA Kumkabidhi AliKiba Tuzo ya BEST AFRICAN ACT, Iliyotolewa Kimakosa Kwa Wizkid
MTV
Europe music Awards 2016 iliyofanyika weekend iliyopita
ambapo Mtanzania mwimbaji staa wa bongofleva Alikiba alikua akiwania tuzo ya BEST
AFRICAN ACT.
Kwenye Kipegele hicho cha Tuzo hiyo aliyetangazwa kuwa mshindi ni Mnigeria
Wizkid.
Pamoja na kwamba Wizkid alitangazwa mshindi, mtandaoni ilikua
inaonyesha Alikiba ndio
anaongoza kwa kupigiwa kura nyingi.
Kutokana na sintofahamu hiyo watu wakaanza kuuliza kwa nguvu imekuaje Ushindi huo kupewa asiyestahili?
Taarifa za Uhakika Kutoka Kwenye Menejimenti ya Alikiba ni kwamba wametumiwa taarifa na MTV
EMA kwamba kuna
kosa lilitokea lakini wamerekebisha na kumfikishia taarifa Wizkid kwamba tuzo
haikuwa yake hivyo itachukuliwa na kupewa Alikiba.
Source Millard Ayo


Post a Comment