Header Ads

Maonesho ya Wakulima na Wafugaji yafanyika Mkoani KILIMANJARO

Mgeni Rasmi katika maonesho ya Wakulima na Wagaji ,Mkuu wa idara ya Utumishi na Utawala Manispaa ya Moshi,Wencelaus Lindi akisoma hotuba ya ufunguzi wa maonesho hayo yaliyoandaliwa na Mtandao wa kusaidia Wakulima wa AgriProFocus yanayofanyika katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika mjini Moshi. 

Baadhi ya wananchi wakiwemo wakulima na wafugaji waliohudhuria ufunguzi wa maonesho hayo ya siku Mbili.

Afisa Msaidizi wa  Mtandao wa wadau mbalimbali wanaosaidia wakulima wenye ndoto wa AgriProFocus ,Hildagard Okoth akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Wenceslaus Lindi wakati akitembelea mabanda katika maonesho ya Wakulima na Wafugaji yanayoendelea katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika Moshi.

Afisa Ugavi wa SEVIA,Lewis Mlekwa akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi alipotembelea banda la taasisi hiyo katika maonesho ya Wakulima na Wafugaji yanayoendelea katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara mjini Moshi.

Bwana Shamba wa kampuni ya Agrichem Africatz Ltd ,Mrisho Yusuph akimuonesha mgeni rasmi baadhi ya mbegu zinazotolewa na kampuni hiyo kwa ajili ya wakulima.

Mgeni rasmi akiwa katika banda la East West Seed akipewa maelezo juu ya aina mbalimbali ya mbegu zinazotolewa na kikundi hicho.

Meneja Mradi mkazi wa Farm Radio International ,Joseph Sarakikya akiomuonesha mgeni rasmi namna radio zinavyoweza kutumika katika kusaidia wakulima.

Afisa mahusiano wa taasisi ya fedha ya Vision Fund ,Elias Mlaki akitoa maelezo kwa mgeni rasmi mara baada ya kutembelea banda la taasisi hiyo.

Afisa Msaidizi wa Mtandao wa wadau mbalimbali wanaosaidia wakulima wenye ndoto wa AgriProFocus akizungumza na wanahabari mara baada ya uzinduzi wa maonesho hayo.

No comments

Powered by Blogger.