Header Ads

Meya aahidi Zawadi kwa Wanaoua Wahalifu

 Meya wa jiji moja nchini Ufilipino ameahidi zawadi kwa watu wanakaowaua au kuwaumiza wahalifu.
Tomas Osmena, aliyechaguliwa kuwa meya mpya wa jiji la Cebu, ameahidi kutoa zaidi ya dola 1,000 kwa kila mshukiwa anayeuawa.
Amesema lengo kuu ni kuzua hofu na wasiwasi miongoni mwa wahalifu.
Bw Osmena tayari amemzawadi polisi ambaye hakuwa kwenye zamu aliyewapiga risasi na kuwajeruhi washukiwa wawili wakati wa jaribio la wizi.

Mpango wa meya hiyo unakaribiana sana na msimamo wa Rais mteule Rodrigo Duterte ambaye ameahidi kutoa amri ya kuuawa kwa wahalifu kama njia ya kukabiliana na uhalifu.

No comments

Powered by Blogger.